Tuesday, January 29, 2013

WILAYA YA IRAMBA KUANZISHA CHUO KIKUU


 Mkuu wa wiilaya ya Iramba Bw. Yahaya Nawanda (katikati) akitsoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha mwaka 2005 hadi 2012. Kushoto ni Mbunge wa Iramba Mwigulu Nchemba na kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba Bi. Christine Midello.


Serikali kwa kushirikiana na kanisa la kiinjili la kirutheli Tanzania dayosisi ya Kati wameanzisha mchakato wa kujenga chuo kikuu katika mji wa Kiomboi wilayani Iramba

Mkuu wa wilaya ya Iramba Bw. Yahaya nawanda amebainisha hayo jana katika taarifa yake ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005/2012

Ameeleza kuwa kwa mwaka wa masomo wa 2013/2014 chuo hicho kitaanza kudahili wanachuo wa shahada ya kwanza ya ualimu kwa ajili ya chuo kikuu Kiomboi Iramba.

Bw. Nawanda amesema kuanzishwa kwa chuo kikuu mkoani Singida kutasaidia kukuza kiwango cha taaluma kwa shule za msingi na sekondari pamoja na kuongeza uwezekano wa ajira kwa vijana.

No comments: