Monday, January 14, 2013

WAANDISHI WA HABARI WAASWA



Na Edilitruda Chami

Wito umetolewa kwa waandishi wa habari mkoani Singida kutumia kalamu zao vizuri na kuepuka uchochezi katika taarifa mbalimbali ili kujenga nchi kwa amani na utulivu

Wito huo umetolewaa ma kamanda wa mkoa wa Singida A.C.P Linus Sinzumwa katika tafrija ya jeshi la polisi na waandishi wa habari iliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Singida

Amesema ni vyema habari zinazopatikana za kiuhalifu ama za kisiasa zikafanyiwa uchambuzi yakinifu kabla ya kutangazawa au kuchapishwa

Amesisitiza kuwa  waandishi ni kichecheo cha maendeleo na kwamba habari zinaweza kujenga au kubomoa amani ya nchi pale kalamu zao zinapotumika  kinyume

Aidha amezitaja nchi za Misri na Libya kama mifano ya nchi za afrika ambazo serikali zao zimepinduliwa kwa kupitia nyanja za mawasiliano ya habari na kwamba waandishi wasisite kutoa taarifa katika vituo vya polisi pale wanapopata vitisho vya namna yoyote  ili hatua zichukuliwe mara moja

No comments: