Monday, January 21, 2013

KANISA LA ANGLIKANA LAKIRI KUKABILIWA NA UKATA



Waumini wa kanisa la Anglikana mjini Singida leo wamekumbushwa  kuwa kutoa sadaka ni sehemu ya ibada.

 

Akihubiri katika kanisa la Anglikana la Mtakatifu Paulo, mwinjilisti Musa Njagamba amesema awali kanisa hilo lilitegemea misaada kutoka kwa wafadhili hivyo waumini wanapaswa kujenga tabia ya kutokuwa tegemezi bali wanapaswa kujitolea ili kuliendeleza kanisa lao.

 

Amesema neno la Mungu halihitaji msaada kutoka nje bali waumini wanapaswa kubadili mienendo kwa kutoa sadaka ili kanisa hilo liweze kujiendesha lenyewe.

1 comment:

Prosper Ngairo said...

Nadhani waumini wanapaswa watambuwe kuwa ni juhudi zao pekee zitakazisaidia kuondoa ukata unalikabili kanisa lao.Kwa hiyo ni vema wakajipanga.
Wajia
Dsm.