Friday, January 18, 2013

POLISI SINGIDA WAPATA PIKIPIKI KUIMARISHA ULINZI


 
 
 
 
 
 
 
 
ACP Linus Sinzumwa Kamanda wa polisi mkoa wa Singida
 
 
 
 
Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Said Mwema ametoa jumla ya piki piki 22 kwa jeshi la polisi mkoani Singida, kama sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa kuimarisha ulinzi nchini na kusogeza huduma za usalama jirani na wananchi

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari mkuu wa jeshi la polisi mkoa wa Singida ACP Linus Sinzumwa amebainisha kuwa pikipiki hizo zitasambazwa katika tarafa za mkoa huo

Kamanda Sinzumwa amebainisha kuwa piki piki hizo zitakabidhiwa kwa askari wateule ambao watazitumia kwa ajili ya kufanya doria na kuzuia uharifu katika tarafa ambazo watapangiwa pamoja na kuimarisha ushirikiano baina ya raia na jeshi hilo

Mkuu wa mkoa wa Singida Dr. Parseko Kone, anatarajiwa kukabidhi vyombo hivyo vya usafiri kwa jeshi hilo mapema wiki ijayo

No comments: