Friday, January 25, 2013

PARACHUTI KUTUMIKA MLIMA KILIMANJARO


Wakazi waishio jirani na mlima Kilimanjaro watanufaika na utalii wa kuruka milima kwa maparachuti utakaofanyika kwa mara ya kwanza nchini, mwezi februari mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari, afisa habari wa mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanapa Bw. Pascal Shelitete amesema fedha zitakazopatikana kupitia utalii huo zitabaki nchini na wananchi waishio jirani na mlima Kilimanjaro watanufaika kupitia mradi wa utunzaji mazingira.

Mradi huo ni pamoja na shughuli zinazohusu masuala ya virusi vya ukimwi, mradi wa maji safi na salama chini ya asasi za one foundation, water International, na plant purpose.

Tukio hilo linatarajiwa kukusanya zaidi ya watalii mia moja kutoka nchi ishirini na tano duniani, na imelenga kukusanya takribani shilingi bilioni mbili za Kitanzania.

 

No comments: