Thursday, May 23, 2013

DW WATOA UDHAMINI KWA STANDARD RADIO FM- USHIRIKIANO WAANZA


Shirika la utangazaji la Ujerumani DW limetoa vifaa vya mawasiiano na utangazaji kwa Standard Radio FM, kama sehemu ya kujenga ushirikiano wa kihabari baina ya Radio za kimataifa Radio za kijamii barani afrika.

Vifaa hivyo vyenye thamani ya zaidi ya dola za kimarekani 300 vimetolewa mwezi april mwaka huu na standard radio imeanza kuvitumia kuunganisha matangazo ya DW na wasikilizaji wa Standard Radio FM

Sambamba na hayo Standard Radio iliyoko mkoani Singida imetiliana saini ya ushirikiano wa muda mrefu wa kihabari na DW na upo mkakati wa wafanyakazi wa SR fm hususani waandishi wa habari na watangazaji kuanza kupata mafunzo yanayotolewa na kituo cha mafunzo ya kitaaluma cha DW kijulikanacho kama Deutch welle Ackademie

Standard Radio iliyoanza matangazo yake mwezi January mwaka huu imekuwa kwa kasi kufuatia kuwa na mikakati kabambe ya kuhakikisha inakuwa Radio Bora katika eneo la Tanzania na maziwa makuu

STANDARD RADIO AUDIENCE- THIS WEEK


Pageviews by Countries

Entry
Pageviews
Tanzania
157
United States
132
Canada
16
Germany
7
France
7
United Kingdom
7
Brazil
6
South Korea
3
Russia
3
India
2

Pageviews by Browsers

Entry
Pageviews
Firefox
123 (26%)
Opera
118 (25%)
Chrome
115 (25%)
Internet Explorer
74 (16%)
Safari
19 (4%)
Mobile Safari
8 (1%)
Dolfin
1 (<1%)
OS;FBSV
1 (<1%)

 

 
 

 

BBC YABISHA HODI STANDARD RADIO FM - MCHAKATO WA USHIRIKIANO WAANZA


Na Boniface Mpagape.

 
Standard Radio FM iliyopo mjini Singida, imeanza mchakato wa kushirikiana na Shirika la utangazaji la Uingereza BBC katika kurusha baadhi ya vipindi na matangazo kutoka shirika hilo.

Hali hiyo imedhihirika baada ya Shirika la BBC Media Action kutuma afisa utafiti wake Bi. Suzy Matamwa ambaye kulingana na maelezo yake mbele ya watumishi wa Standard radio atakuwa na mazungumzo ya ana kwa ana na kila mwandishi kuhusiana na shughuli za kila siku zinazofanyika katika masuala mbali mbali ya uandaaji wa habari na vipindi mbalimbali.

 


 PIC 1. Bi. Suzy Matama akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Standard Radio katika ofisi za SR FM. Kutoka kulia ni Meneja wa SR Bw. Prosper Kwigize, Mkurugenzi wa SR Bw. James Daud na Bi. Suzy Matama kutoka BBC Media Action, wakati akitambulishwa rasmi.


Naye meneja wa Standard radio Bw. Prosper Kwigize amesema kuwa Standard radio inatangaza vipindi mbali mbali vinavyoigusa jamii moja kwa moja katika nyanja mbali mbali zikiwemo za afya, elimu, kilimo, uchumi, ambavyo hutangazwa na redio hiyo.

Aidha amesema standard radio imekuwa ikipokea wanafunzi kutoka vyuo mbali mbali vya uandishi wa habari hapa nchini.
 
Amesema hivi sasa kuna wanafunzi wanne waliopo katika mafunzo kazini na kwamba wengine waliokuwepo wamemaliza muda wao na kurejea kwao na kwamba zaidi ya wanafunzi watango kutoka chuo kikuu cha mtakatifu Augustino cha jijini Mwanza wanatarajia kuanza mafunzo kwa vitendo ndani ya Standard radio hivi karibuni

Afisa utafiti huyo kutoka shirika la BBC Media Action, amesema atakuwa akizungumza na wafanyakazi wa standard radio kwa nyakati tofauti kwa muda wa siku tatu, kuhusu masuala ya kawaida kama uandaaji wa vipindi, habari na kurusha matangazo kwa ujumla.

Endapo mpango huo utafanikiwa itakuwa ni fursa nzuri kwa wakazi wa Singida kuweza kusikika katika ngazi ya kimataifa kupitia BBC kwani nao pia watapata fursa ya kuchangia maoni yao kuhusu masuala mbali mbali katika jamii.

Watumishi wa Standard radio pia watanufaika kwa kupatiwa mafunzo pamoja na vitendea kazi ili kuwezesha ufanisi katika kazi za kila siku za kuhabarisha na kuelimisha jamii.

 


PIC 2. Meneja wa SR FM Bw. Prosper Kwigize (Katikati) akitambulisha baadhi ya wafanyakazi wa standard radio kwa mgeni kutoka BBC Media Action.  Kulia kwake ni mtangazaji na mwandaaji wa vipindi Bw. Cales Katemana na kushoto kwake ni fundi mitambo wa SR Bw. Moses Anthony.

 

 PIC 3. Mtafiti kutoka BBC Media Action Bi. Matama (aliyeinama kulia) akisikiliza kwa makini majina ya wafanyakazi wa SR bali pia kutaka kujua kila mmoja anafananaje,  wakati wakitambulisha kwake. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa SR. Bw. James Daud.

Saturday, May 18, 2013

WASOMI KUTOKA KIGOMA WALIA NA WABUNGE WAO



Wabunge wa mkoa wa Kigoma wamehimizwa kujenga umoja na kuwa na mkakati maalumu wa kuutetea mkoa wa Kigoma na kuepuka ushabiki wa kisiasa ambao unatajwa kuiangamiza Tanzania
 
 
 
Raia hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Amos Nyandwi (pichani hapo juu) mchumi kutoka wizara ya kazi na ajira ambaye pia ni mwenyeji wa mkoa wa Kigoma katika kongamano la vijana wasomi kutoka vyuo mbalimbali nchini ambao ni wazawa wa Kigoma
 
Bw. Nyandwi amebainisha kuwa kwa sasa wabunge wote wa majimbo na viti maalumu kutoka mkoa wa kigoma  hawajaonesha umahili wao katika kubuni na kusimamia mipango ya maendeleo kwa njia ya umoja kama wawakilishi wa wanakigoma Bungeni
 
Amesisitiza kuwa licha ya kuwepo na wataalam walioajiliwa serikalini na katika sekta binafsi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakisaidia kuchochea wabunge hao kuungana na kuwatumia wataalamu kuibua na kusimamia maendeleo lakini hakuna mwitikio wa wabunge hao
 
Aidha Nyandwi ameonya juu ya wanasiasa kung’ang’ana na vyma vya siasa na kushindwa kusimamia maslahi ya wananchi ambao ndio waliowapigia kura
 
Pamoja na lawama hizo kwa wabunge na wanasiasa, mchumi huyo amewahimiza wasomi walioko katika vyuo kufikiri kurejea mkoani Kigoma na kuunda au kujiunga na vikundi vya ujasiriamali ii kunufaika na mipango ya serikali ya uwezeshaji jamii kiuchumi.
 
 
 
Kwa upande wake mkurugenzi wa makampuni ya Buhanzo na Standard Voice limited Bw. James Japhet (pichani hapo juu) amewaonya wasomi kutoka Kigoma kuondoa fikra za kutaka kuajiriwa badala yake wasome kwa umakini na watumie alimu yao kwa ajili ya ujasiriamali
 
Bw. Japhet ameongeza kuwa mkoa wa Kigoma una vyanzo vingi vya uchumi ambavyo havijatumika kuwainua wakazi wa mkkoa wa Kigoma hususani mazao ya ziwa Tanganyika, kilimo, ufugaji na fursa za biashara katika mipaka ya nchi jirani za Burundi, DRC na Zambia.
 
Aidha Bw. Japhet amewataka wabunge wa mkoa wa Kigoma kuungana pamoja kutetea ujenzi wa barabara pamoja na mkoa kuunganishwa na umeme wa gridi ya taifa, na kwamba bila miundombinu ya umeme na barabara za uhakika Kigoma haitapata maendeleo endelevu.
 
 
Zaidi ya wanafunzi 80 kutoka vyuo vya SAUT, Udom, SUA, Mzumbe, St. John, RUAHA na Tumaini wamehudhuria kongamano hilo, ambapo ni mbunge mmoja tu kutoka jimbo la Muhambwe Bw. Felix Mkosamali (pichani aliyekaa katikati juu) aliyejitokeza kushiriki.

Tuesday, May 7, 2013

MAALIM SEIF SHARIF HAMAD AZURU MKOA WA SINGIDA

MAKAMU wa kwanza wa Rais, Serikali ya mapinduzi Zanzibar Seif Sharif Hamadi amewataka Watanzania kudumisha upendo baina yao ili kuepuka chuki zinazoanza kujitokeza sasa nchini, kiasi cha kusababisha vurugu na vifo kwa wananchi wasiyo na hatia.
Maalimu Seif amesema hayo mjini Singida, kwenye ziara yake ya siku mbili mkoani humo iliyoanza May 06 2013 ambapo alipokelewa na viongozi wa serikali na chama cha wananchi CUF mkoani humo.
katika hotuba yake Bw. Seif amesema Watanzania siku zote wamekuwa ni watu wa amani, lakini vurugu zinazoanza kujitokeza sasa siyo za kistaarabu na zinaashiria kuna watu wanaochochea ili kufanikisha malengo waliyokusudia.
Alitumia fursa hiyo kuitaka serikali ya Tanzania kufuatilia kwa makini tukio la ulipuaji bomu katika ibada ya ufunguzi wa kanisa katoliki la Mtakatifu Joseph mkoani Arusha, ili waliohusika wote wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
 
PICHA: Mkuu wa wilaya ya Singida Mwl. Queen Mlozi akimkaribisha jukwaani Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar ili kumpa fursa ya kuhutubia umati wa wananchi mjini Singida
 
Aidha alilaani shanbulio hilo la bomu kuiomba Serikali iendelee kulinda usalama wa wananchi wake kwa ajili ya kuenzi misingi imara ya amani, umoja na upendo iliyoasisiwa na waazilishi wa  Taifa la Tanzania.
Makamu wa kwanza wa Rais Seif Sharif Hamad alimaliza ziara yake jana na alitarajiwa kuondoka mkoani Singida ili kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa.

Sunday, May 5, 2013

MAALBINO WALINDWE NA KUTAMINIWA NA JAMII




Mkuu wa Mkoa wa Singida Bw Pareseko Kone Ameshukuru Serikali na chama cha Walemavu wa ngozi Tanzania kwa kuupa heshima ya kuwa wenyeji wa maazimisho ya siku ya ualbino kitaifa  mkoa wa Singida.

 

Kauli hiyo imesema wakati wamaadhimisho ya siku ya Albino kitaifa yaliyofanyika jana katika uwanja wa  Namfua  Mkoani Singida.

 

Bw. Kone ameeleza kuwa wizara husika na chama cha walemavu wa ngozi Tanzania walijadili na kuamuwa kuwa Mkoa wa Singida ni moja kati ya mikoa inayoweza kuanda na kufanikisha shughuli hizo.


Aidha Bw Kone ameeleza kuwa kuwa kauli mbiu ya mwaka huu katika  maadhimisho hayo ni Kansa ya Ngozi Je Waijuwa, na mkoa wa wamejipanga kuhakikisha kuwa kila mlemavu wa ngozi anapata huduma iliyo ndani ya uwezo wa mkoa.

SIKU YA WALEMAVU WA NGOZI-ALBINO TANZANIA

Tuwalende na kuwajali wenye ulemavu




Wito Umetolewa kwa kila halmashauli ya Tanzania kuwa na bageti maalum kwa ilikuweza kuwawezesha watu wenye ulemavu wa ngozi kupata tiba kwa muda muafaka na kuwapatia huduma mbali mbali za kijamii

 

Kauliyo hiyo imesemwa na waziri wa tawala za mikoa na serikali za mitaa kutoka offisi ya waziri mkuu Bi. Hawa Ghasia katika kiwanja cha Namfua mkaoni Singida wakati wa maazimisho ya siku ya albino Kitaifa

 

Bi Hawa ameeleza kuwa  Halmashauli zinapaswa kufuatilia sensa iliyofanya ilikuweza kuwa na idadi kamili  ya watu hao ilikuweza kuwa na mgawanyo mzuri na utakao wawezesha wapeleka huduma kuwa na ufanisi wa kuwafikishia huduma kwa muda muafaka.

 

 

Aidha Bi Hawa amelani na kukemea Vitendo vya mauaji na kuwanyanya paa walemavu kuwa ni vitendo vya kikatili na atakaye bainika kufaya hivyo hatua kali za kisheria  zita chukuliwa.

 

 
 
 
 
 



Thursday, May 2, 2013

BONANZA LA STANDARD RADIO MEI MOSI 2013- MATUKIO KATIKA PICHA

Timu ya soka ya Standard Radio katika picha ya pamoja kabla ya mechi kati yao na mashabiki na wapenzi wa radio hiyo ijulikanayo kama STANDARD RADIO SALAAM CLUB FC muda mfupi kabla ya kuanza kwa mpambano ambao hata hivyo hakukuwa na mbabe baada ya timu zote kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja, mpambano huo ulichezwa katika uwanja wa ufukwe wa Ziwa Kindai mjini SIngida
 
 
Meneja wa Standard Radio Bw. Prosper Kwigize akisikilliza maelekezo ya kocha muda mfupi kabla ya mechi kuanza, Kwigize kutoka winga ya kulia ndiye aliyetoa pasi iliyosababisha kupatikana kwa bao la kusawazisha kipindi cha pili, mbele aliyeshika nyonga ni mchezaji centre half Imani Msigwa



























Kikosi cha Standard Radio FC kikijipanga kuzuia mpira wa adhabu kutoka kwa wapinzani wake STANDARD salaam club FC, Mwenye jezi namba 13 mgongoni ni mwanaspoti wetu Cales Katemana na jezi namba 12 ni Abdul Bandola  mtayarishaji msaidizi wa kipindi cha Michezo kinachorushwa na standard radio kila siku saa moja na nusu jioni



























Abdul Bandola (kulia menye bukta ya njano) star wa Standard Radio fc akichapa mwendo kufunga bao la ushindi, hata hivyo walinda mlango wa Salaam Club FC walifanikiwa kuzuia mashambulizi.

Meneja wa Standard Radio akiongoza kikosi cha mashabikii na watangazaji kuelekea uwanjani tayari kwa mtifuano wa Bonanza la Standard radio na Mei Mosi, Standard Radio Imeahidi kuendesha matamasha mbalimbali pamoja na mashindano ya soka kwa wanaume na wanawake kama sehemu ya kuitangaza Radio hiyo, Hivi karibuni lilifanyika tamasha kubwa na zuri wilayani Ikungi na inatarajiwa kufanyika tena mjini Singida na Iramba kabla ya kuenlekea Igunga na Nzega mkoani Taboba na baadaye matamasha hayo yatafanyika katika wilaya za Hanang na Mbulu mkoani Manyara

Bw. Boniface Mpagape (mwenye koti) ambaye ni Mhariri wa Standard Radio ambaye ni Mhariri akiongoza kikosi cha pili cha soka kutoka SR FM kuelekea uwanjani muda mfupi kabla ya mechi hiyo kuanza, Mpagape a.k.a Furgason) ndiye Kocha mchezaji wa timu ya soka ya Standard Radio

Wednesday, May 1, 2013

HELVETAS USWISS YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA STANDARD RADIO

Maafisa wa shirika la maendeleo la Uswiss wakizuru ofisi na jumba la matangazo la Standard Radio mkoani Singida katika ziara yao maalumu ya kutembelea kituoo hicho kwa malengo ya kuandaa mkakati wa kuanzisha ushirikiano katika kuandaa vipindi vya maendeleo hususani katika kilimo na ufugaji

katika kipicha kutoka kushoto Bw. Christian Bobst mpiga picha kutoka nchini Uswiss, Bi. Astrid Rana na Bi. Franca Palmy maafisa wa Helvetas wanaohusika na masuala ua ushirikiano na utunishaji wa mfuko wa maendeleo kwa ukanda wa Afrika na mwenye suti nyeusi ni Bw. Prosper Kwigize Meneja wa Standard Radio

katika picha ni Bw. Yusuph Salum mratibu wa shirika la Helvetas mkoanii Singida akiwa na Maafisa wake kutoka nchini Uswiss katika studio za Standard Radio, walikuwa wakishuhudia mafumo wa matangazo na namna matangazo yanavyorushwa na mtangazazji wa zamu

STANDARD WATOA FURSA YA MAFUNZO KWA VITENDO




























Kituo cha matangazo cha Standard Radio fm, kimepokea wanafunzi kutoka vyuoo mbalimali vya habari nchini kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo katika kipindi cha May-July mwaka huu

 

Waliopokelewa ni wanafunzi kutoka vyuo vya Musoma Utalii, SAUT na Arusha Journalism ambao pamoja na mambo mengine watashiriki kazi za kihabari na utangazaji

 

Pichani ni baadhi ya wanachuo hao, ambao wamewasili leo Mei Mosi kuanza rasmi mafunzo yao

 

Kutoka kulia ni Bi. FATMA MUNA na MARIAM MATUNDU kutoka Arusha Journalism na Bw. MAZIKU MOTTO kutoka Musoma Utalii Tabora.