Thursday, May 23, 2013

BBC YABISHA HODI STANDARD RADIO FM - MCHAKATO WA USHIRIKIANO WAANZA


Na Boniface Mpagape.

 
Standard Radio FM iliyopo mjini Singida, imeanza mchakato wa kushirikiana na Shirika la utangazaji la Uingereza BBC katika kurusha baadhi ya vipindi na matangazo kutoka shirika hilo.

Hali hiyo imedhihirika baada ya Shirika la BBC Media Action kutuma afisa utafiti wake Bi. Suzy Matamwa ambaye kulingana na maelezo yake mbele ya watumishi wa Standard radio atakuwa na mazungumzo ya ana kwa ana na kila mwandishi kuhusiana na shughuli za kila siku zinazofanyika katika masuala mbali mbali ya uandaaji wa habari na vipindi mbalimbali.

 


 PIC 1. Bi. Suzy Matama akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Standard Radio katika ofisi za SR FM. Kutoka kulia ni Meneja wa SR Bw. Prosper Kwigize, Mkurugenzi wa SR Bw. James Daud na Bi. Suzy Matama kutoka BBC Media Action, wakati akitambulishwa rasmi.


Naye meneja wa Standard radio Bw. Prosper Kwigize amesema kuwa Standard radio inatangaza vipindi mbali mbali vinavyoigusa jamii moja kwa moja katika nyanja mbali mbali zikiwemo za afya, elimu, kilimo, uchumi, ambavyo hutangazwa na redio hiyo.

Aidha amesema standard radio imekuwa ikipokea wanafunzi kutoka vyuo mbali mbali vya uandishi wa habari hapa nchini.
 
Amesema hivi sasa kuna wanafunzi wanne waliopo katika mafunzo kazini na kwamba wengine waliokuwepo wamemaliza muda wao na kurejea kwao na kwamba zaidi ya wanafunzi watango kutoka chuo kikuu cha mtakatifu Augustino cha jijini Mwanza wanatarajia kuanza mafunzo kwa vitendo ndani ya Standard radio hivi karibuni

Afisa utafiti huyo kutoka shirika la BBC Media Action, amesema atakuwa akizungumza na wafanyakazi wa standard radio kwa nyakati tofauti kwa muda wa siku tatu, kuhusu masuala ya kawaida kama uandaaji wa vipindi, habari na kurusha matangazo kwa ujumla.

Endapo mpango huo utafanikiwa itakuwa ni fursa nzuri kwa wakazi wa Singida kuweza kusikika katika ngazi ya kimataifa kupitia BBC kwani nao pia watapata fursa ya kuchangia maoni yao kuhusu masuala mbali mbali katika jamii.

Watumishi wa Standard radio pia watanufaika kwa kupatiwa mafunzo pamoja na vitendea kazi ili kuwezesha ufanisi katika kazi za kila siku za kuhabarisha na kuelimisha jamii.

 


PIC 2. Meneja wa SR FM Bw. Prosper Kwigize (Katikati) akitambulisha baadhi ya wafanyakazi wa standard radio kwa mgeni kutoka BBC Media Action.  Kulia kwake ni mtangazaji na mwandaaji wa vipindi Bw. Cales Katemana na kushoto kwake ni fundi mitambo wa SR Bw. Moses Anthony.

 

 PIC 3. Mtafiti kutoka BBC Media Action Bi. Matama (aliyeinama kulia) akisikiliza kwa makini majina ya wafanyakazi wa SR bali pia kutaka kujua kila mmoja anafananaje,  wakati wakitambulisha kwake. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa SR. Bw. James Daud.

No comments: