Thursday, March 28, 2013

TAARIFA YA HABARI KUTOKA STANDARD RADIO


Source; SR/ Neema J

Ed;

Date; March, 27, 2013

 

SINGIDA

Mkuu wa wilaya ya singida  Bi Queen Mlozi,  amelita jeshi la polisi  kutumia mafunzo watayoyapata  ipasavyo,  na kusema yatawasaidia kuongeza maarifa mapya  na kuleta  mabadiliko,  kwa kuwajibika  katika utendaji kazi wao.

Akizungumza katika uzinduzi wa mafunzo ya jeshi polisi kazini jana Bi Mlozi amesema, maendeleo hayawezi kuja bila changamoto, hivyo  kuwataka polisi  kuhamasishana  katika utendaji kazi wao,   bila kukata tamaa kwani elimu haina mwisho.

Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP Linus Sinzumwa, amesema lengo la mafunzo hayo  kutawezesha  afisa  askari  na polisi  ufanisi wa kufanya kazi,  kuleta mabadiliko katika utendaji  kazi wao,  pamoja na kuliwezesha jeshi la polisi kufanya kazi kwa  ufanisi, usasa,  uweledi  pamoja kushirikishaisha jamii, juu ya ulinzi  wa mali zao.

Naye mkufunzi wa   elimu ya watu wazima mkoa wa singida Bw Musa Nkungu,  ambaye ni mmoja  kati ya  watoa mafunzo  kwa jeshi la polisi,  amesema  mafunzo hayo yatawasaidia polisi kupata mafaniko,  ikiwa ni pamoja na  muhitimu   kutunikiwa cheti atakapo hitimu  mafunzo kazini,  na kupandishwa cheo  na kuongezewa madaraka  ya uongozi, katika jeshi la polisi  hivyo kuwataka polisi kuhudhuria katika mafunzo, ili waongeze ufanisi wa kazi .

 

Source; Tanzania Daima

Ed;

Date; March, 27, 2013

DAR ES SALAAM

Serikali imesema haitamvumilia mtu atakayeendesha shughuli za kibinadamu, katika maeneo tengefu  lengo ni kunusuru ikolojia ya Hifadhi za Serengeti, Ngorongoro na Loliondo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, amesema wananchi walioingia ndani ya pori tengefu la Loliondo, wanatakiwa kuondoka mara moja.

Balozi Khagasheki amesema kutokana na mgogoro ulioko Loliondo kwa muda mrefu sasa, serikali imepata ufumbuzi ambapo wananchi wanatakiwa kutii sheria bila kushurutishwa.

Aidha amesema ili, kutatua migogoro iliyopo serikali itatenga na kuchukua sehemu ya ardhi ya Pori Tengefu la Loliondo, yenye ukubwa wa kilomita za mraba 1500 kutoka kwenye eneo la kilomita za mraba 4000, za pori hilo.

Source; SR/ Elizabeth, Martine

Ed;

Date; March, 27, 2013

 

SINGIDA

Wanachama wa chama cha walemavu wasiioona mkoani Singida TLB, wanakabiliwa na changamoto mbalimbali katika maisha yao ya kila siku, na kusababisha kushindwa kutekekeleza majukumu yao.

Akizungumza na standard radio mwenyekiti wa chama cha walemavu wa kutoona mkoani singida Bw. Hassani kingugu , ambaye pia ni mlemavu wa kutoona amesema kuwa, changamoto zimekuwa ni tatizo katika maisha yao jambo linalopelekea wao kushindwa kumudu maisha, na kubaki wanahangaika.

Bw. Kingugu amezitaja changamoto hizo kuwa  ni jamii kuwa na mtazamo hasi kwa kudhani walemavu hawawezi kitu, uhaba wa shule, vifaa vya kujifunzia na kufundishia, kubadilika kwa mitaala, kutoshirikishwa kwenye shughuli za ujasiriamali, pamoja na viongozi mbalimbali kutowaelimisha wanajamii, namna ya kuwajali na kuwahudumia walemavu wasioona.

Aidha ametoa wito kwa jamii kutowabagua walemavu na badala yake itambue mchango wao katika maisha ya kila siku, kwani kuna walimu ,wafanyabiashara, mahakimu ambao ni walemavu.

Source; Tanzania Daima

Ed;

Date; March, 27, 2013

TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni mstaafu Chiku Galawa, amesema tatizo la vijana wengi kukosa ajira linaweza kumalizika ikiwa watavitumia vyuo vya ufundi stadi (VETA), vilivyopo katika maeneo yao.

Mkuu huyo wa mkoa ametoa kauli hiyo katika ziara yake ya kutembelea chuo cha Veta cha jijini Tanga, kwa lengo la kujua hatma ya vijana hao, kupatiwa nafasi mbalimbali, ili hatimaye waondokane na tabia ya kurandaranda mitaani.

Galawa ametumia fursa hiyo kuwataka vijana kutambua fursa hiyo, akiwahakikishia kwamba wanaweza kujikwamua na suala la umaskini, linalowakabili vijana wengi, kutokana na kukosa shughuli za kufanya.
Naye Mkurugenzi wa Chuo cha Ufundi Veta Tanga, Alphonce Kibasha, amemwambia mkuu wa mkoa kwamba changamoto inayowakabili ni uhaba wa majengo, ya kuweza kuchukua vijana wengi kwa wakati mmoja.

Monday, March 25, 2013

HABARI KUTOKA STANDARD RADIO FM 90.1 MHz

Source:SR/E. Lyatuu.

Ed: BM

Date: March 25, 2013.

 

SINGIDA

Jamii katika manispaa ya Singida, imetakiwa kutoona vijana ni mzigo badala yake ione kuwa vijana ni suluhisho la kuleta mabadiliko ya kimaendeleo katika nchi, ili kuondokana na umaskini kwa kuwa vijana ni nguzo ya taifa.

 

Bw. Fidelis Yunde Mratibu na mwanzilishi wa shirika la harakati za vijana katika kuleta maendeleo, Youth Movement for Change YMC amesema hayo, wakati akizungumza na standard radio ofisini kwake, kuhusiana na fursa za vijana katika jamii, mapema leo.

 

Bw. Yunde amesema jamii inapaswa kuwapa vijana hamasa kwa kuwahamasisha, kuwapa nafasi mbali mbali za uongozi kwa kuamini wanaweza, kama vile uongozi katika siasa, kwani wao ni mabalozi wazuri katika vita dhidi ya umaskini.

 

Aidha, amewataka vijana kuunda vikundi mbali mbali kama vile vya kiutamaduni, ujasiriamali, ili kujua jinsi ya kubuni, kuanzisha na kuboresha biashara kwa kupata elimu kuhusu maendeleo ya vijana, na kuchukua hatua kubadili vijiwe vyao kuwa vijiwe vya kazi ili kuleta maendeleo. Amesema vijana wajitume kwa kujishughulisha katika fursa zilizopo kama vile kilimo kwanza, pia viongozi wawekeze zaidi kwa vijana kwa kutoa nafasi za uongozi.

 


Source:Tanzania Daima

Ed: BM

Date: March 25, 2013.

DAR ES SALAAM

Meneja wa wafanyakazi wa ndani ya ndege wa Kampuni ya FastJet, Emma Donavan anayedaiwa kutoa lugha ya matusi kwa mfanyakazi mwenzake, leo amefikishwa mahakamani.

Donavan amefikishwa mahakamani baada ya polisi kukamilisha kazi ya kumhoji sambamba na mashahidi wengine na kisha jalada lake kufikishwa kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini DPP, ambaye naye baada kumaliza kulipitia alilirudisha polisi, ili taratibu za kwenda mahakamani ziendelee.

Meneja huyo anakabiliwa na tuhuma za kutoa lugha ya matusi kwa mfanyakazi mwenzake, Samson Itembe. Wiki iliyopita, Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege, Deusdedit Kato, alisema walimaliza kumhoji Emma na jalada kupelekwa kwa DPP.

Habari kutoka Kituo cha Polisi cha Mamlaka ya Viwanja vya Ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu JK Nyerere -Terminal One -  zinasema polisi wamekuwa wakikukusanya ushahidi kutoka kwa wafanyakazi wengine kabla ya jalada kupelekwa kwa DPP.

Meneja huyo ambaye ni raia wa Uingereza alikamatwa wiki iliyopita baada ya kusakwa kwa siku kadhaa.

Source:SR/Bandola.

Ed: BM

Date: March 25, 2013.

 

SINGIDA

Chama Cha Mapinduzi CCM kimewaomba wamiliki halali wa eneo la Nkonkilangi Shelui  katika wilaya ya Iramba mkoani Singida, kuwaruhusu wachimbaji wadogo wadogo wasio na leseni kuendelea kuchimba ili kujipatia riziki.

 

Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Singida Bw. Mgana Msindai wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za chama hicho mkoani humu.

 

Bw. Msindai amesema kuwa wachimbaji wadogo wadogo wasio na leseni ndiyo walioomba CCM  Mkoa iwasaidie waruhusiwe kuendelea kuchimba na kwenye kikao cha kamati ya siasa mkoa, kilikubaliana chama kisaidie kuwaokoa wananchi wa Nkonkilangi waendelee kujipata riziki zao.

Aidha Bw. Msindai amesema hayo kufuatia mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima  Shehe Semtana aliyeandika kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM mkoani Singida, Bw. Mgana Msindai anatuhumiwa  kupora machimbo ya madini ya wachimbaji wadogo wadogo katika kijiji cha Nkonkilangi na kumkabidhi Bw John Bina bila ridhaa ya wanakijiji.

 

 

Source:SR/Saada

Ed: BM

Date: March 25, 2013.

SINGIDA

Kamishna msaidizi wa madini kanda ya Kati Bw. Manase Mbasha, amewataka wachimbaji wadogo wadogo wa madini kukata leseni, kulingana na maeneo waliyo na uwezo nayo, na kuacha kutegemea wafadhili na wawekezaji.

Bw. Mbasha amesema hayo leo, wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kutokana na umhimu wa wachimbaji kukata leseni kulingana na maeneo waliyo na uwezo nayo, na kuacha kuomba leseni ya kumiliki maeneo makubwa ambayo hawana uwezo wa kuyafanyia kazi.

Aidha, Bw. Mbasha ametaja maeneo yenye wachimbaji wadogo wadogo mkoani Singida kuwa ni, Misigiri, Mpambaa, Msangachuki, Londoni, Sekenke, na Nkonkilangi.

Amesema ofisi yake inakaribia kutoa leseni kwa wachimbaji wa madini ya shaba, chumvi, zilikoni, na madini ya chuma.


Source:SR/Saada

Ed: BM

Date: March 25, 2013.

 

DAR ES SALAAM

Rais wa China Xi Jinping leo amehutubia dunia kutokea nchini Tanzania kuelezea sera ya serikali ya China kwa Bara la Afrika.

Hotuba hiyo imetolewa mara baada ya kuzindua na kukabidhi rasmi kituo cha mikutano cha kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es salaam kilichojengwa kwa msaada wa serikali ya China kwa lengo la kumuenzi Mwalimu Nyerere.

Rais huyo wa China amesaini mikataba kumi na saba na rais Jakaya Kikwete, na baadaye ametembelea makaburi ya wataalam wa kichina yaliyopo katika kijiji cha Majohe-Ukonga, ambapo ametoa heshima zake kwa wachina waliofariki wakati wakijenga reli ya TAZARA.

Rais Xi Jinping ameondoka nchini leo jioni kuelekea nchini Afrika kusini kuhudhuria mkutano wa tano wa wakuu wa nchi za BRICS ambazo ni Brazil, India, China na Afrika kusini.

Friday, March 22, 2013

KAMATI YA BUNGE -TAMISEMI YAPATA HOFU SINGIDA


SINGIDA

Kamati ya bunge tawala za mikoa na serikali za mitaa imeitaka serikali kupitia ofisi ya mkaguzi wa hesabu za serikali kufanya uchunguzi wa matumizi mabaya ya fedha zilizotumika kujenga kibanda cha kuchomea taka katika hospitali mpya ya rufaa mkoani Singida.

 

Akitoa maazimio ya kamati hiyo mara baada ya kupokea taarifa fupi kuhusu ujenzi wa hospitali mpya ya rufaa ya mkoa wa singiga leo, Mwenyekiti wa kamati hiyo Dk Hamisi Kigwangara amesema kibanda hicho, kinaonyesha kugharimu milioni 98 na nne jambo ambalo sio sahihi ikilinganishwa na gharama halisi mara baada ya kuona mradi huo.

 

Amesema mkataba wa ujenzi unaonyesha kuwa bati zilizotumika katika ujenzi zinagharimu milioni kumi huku kukiwa hakuna uhalisia kati ya idadi ya bati na fedha iliyotumika jambo linaloonyesha mapungufu

 

Aidha amesema serikali inatakiwa kutuma fedha za kukamilisha mradi wa ujenzi wa hospitali hiyo ambazo zilipitishwa katika bunge takribani bilioni mbili ili kuharakisha ujezi wa hospitali hiyo

 

Kamati hiyo ya bunge imefanya ziara ya siku mbili mkoani Singida ambapo imekagua miradi pamoja na kuzungumza na sekretarieti ya mkoa na imerejea leo mjini Dodoma


Source: SR/Hawa

Ed: BM

Date;21/3/2013

 

SINGIDA

Jumla ya wahamiaji haramu 30 wameripotiwa kuingia mkoani Singida kwa kipindi cha January  2012 hadi march 2013 kinyume cha sheria.

 

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari afisa uhamiaji mkoa wa Singida

Bw.Adam Mnyeke amesema wahamiaji hao wanatoka katika nchi za Ethiopia,Somalia, Burundi na Kenya na kwamba hupita njia zisizo rasmi.

 

Amesema miongoni mwa wahamiaji hao waethiopia ni 24,wasomali 3, wakenya 2 na mrundi mmoja.

 

Aidha amesema uchunguzi umebaini chanzo cha wahamiaji hao haramu kutoka katika nchi zao kuwenda nchi jirani ni  kutokana na hali ngumu ya maisha, na hali mbaya ya kiusalama katika nchi zao,na hufanya hivyo kunusuru maisha yao

 


Source: SR/Bandola

Ed: BM

Date;21/3/2013

 

SINGIDA

Wito umetolewa kwa wananchi kwa kushirikiana na vikundi vya polisi jamii katika suala la kufanya usafi katika kata ya utemini ndani ya manispaa ya Singida

 

Mtendaji wa kata  hiyo Bw. Noel Hago ametoa wito huo wakati akiongea na Standard Redio leo ofisini kwake.

 

Bw. Hago amesema hayo kufuatia siku iliyopangwa na viongozi kwa kushirikiana na  polisi kata, kufanya usafi siku ya tarehe 22 mwezi 3 mwaka huu.

 

Aidha Bw. Hago amesema wananchi wanapaswa kuonyesha ushirikiano wao dhidi ya viongozi ili kuweza kufanikisha zoezi hilo.

 

 

 


Source: SR/Hawa

Ed: BM

Date;21/3/2013

 

SINGIDA

 Chama cha wafanyabiashara, viwanda,na kilimo mkoani singida  TCCIA  kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa fedha na kukosa wafadhili.

 

Hayo yamesemwa na afisa mtendaji wa chama hicho mkoani singida Bw. Calvert Nkurlu wakati akizungumza na standard radio ofisini kwake.

 

Amesema chama hicho kilianzishwa kwa lengo la kuunganisha nguvu ya wafanyabiashara, viwanda, pamoja na wakulima wawe na sauti moja katika masuala yanayowahusu ili kuendesha biashara kwa ufanisi

 

Aidha chama mkoani Singida kina wanachama mia sita themanini na sita, idadi ambayo ni ndogo ikilinganishwa na wafanyabiashara na wakulima waliopo katika mkoa wa singida

 

Ametoa wito kwa wafanya biashara kutumia mitandao mbalimbali ili kupata habari zinazohusu biashara, kusajili majina ya biashara, pamoja serikali kukaa pamoja na wafanyabiasha ili kujadili hali halisi ya biashara
Source: Tanzania Daima

Ed: BM

Date;21/3/2013

 

BUKOBA

Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba wamedai kuwa Meya wao, Anatory Amani, amekuwa akiendesha shughuli zake kibabe, ikiwa ni pamoja na kuidhinisha matumizi ya fedha bila kuwashirikisha.

Madiwani hao wametoa madai hayo jana mbele ya tume iliyoundwa na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kuchunguza tuhuma za ufisadi wa miradi mitatu zinazomkabili meya huyo, ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro.

Wajumbe wengine mbali na Kandoro ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Rehema Nchimbi, Naibu Katibu Mkuu wa Tamisemi na Naibu Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Madiwani hao kwa nyakati tofauti wameiambia tume kuwa Amani amekuwa mbabe na kufikia hatua ya kuhamisha fedha kutoka mfuko wa mradi wa viwanja sh milioni 200 kwenda kulipia deni la mradi wa soko bila idhini yao.
Source: SR/E. Lyatuu

Ed: BM

Date;21/3/2013

SINGIDA

Wananchi wa kijiji cha Mandewa Kata ya Mandewa manispaa ya Singida, wametakiwa kuwa na subira kuhusu suala la kuhamishwa kwa soko la gineri

 

Mtendaji wa Kata hiyo Bw. Bakari Ntandu amesema hayo wakati akizungumza na standard radio ofisini kwake, kuhusu mikakati iliyopo ya kuhamishwa kwa soko hilo.

 

Amesema eneo linalotumika kama soko, linatumika kwa muda na wala halikupangwa maalum kwa ajili ya soko na kwamba lipo eneo husika kwa ajili hiyo na utaratibu wa kuhamia katika eneo hilo unafanyika.

 

Amesema utaratibu unaofanyika ni kusubiri kampuni ya Spencon kukamilisha mradi wa maji, kwa kuwa eneo lililotengwa kwa ajili ya soko lipo karibu na mradi wa maji unaojengwa.

 
Aidha amewataka wananchi kuwa tayari kuhama katika eneo linatumika kama soko, kwa kuwa si eneo lililotengwa maalum kwa ajili ya biashara, kwa kufuata taratibu na kutoeneza uvumi kuhusu kuhamishwa kwa soko

SINGIDA YALIA NA UHABA WA CHAKULA



Na. Boniface Mpagape.

Mkoa wa Singida umeazimia kuweka kipaumbele kwa mazao yanayostahimili ukame ambayo ni mtama, uwele na viazi vitamu ili kuondokana na tatizo la upungufu wa chakula.

Maazimio hayo yamefikiwa katika kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa VETA mkoni humo. Mwenyekiti wa kikao hicho, mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Ole Kone amesisitiza wakulima kulima mazao yanayostahimili ukame, ili kwenda sambamba na hali ya hewa mkoani Singida, kutokana na ukame unaoukabili mkoa huo.

 

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao hicho Dk. Kone amesema kwa zaidi ya miaka mitatu mkoa umekuwa na ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula kutoka tani 442,180 mwaka 2009/2010 hadi tani 575,228 mwaka 2012, sawa na ongezeko la asilimia 30.

 

Amesema uzalishaji wa mazao ya biashara umeongezeka kutoka tani 164,673 mwaka 2009/2010 hadi tani 289,305 mwaka 2011/12 sawa na ongezeko la asilimia 76, na kwamba mafanikio hayo yanatokana na Mkoa kuteua na kufanya juhudi ya kuendeleza mazao ya kipaumbele kwa kuzingatia hali ya hewa. Ameyataja mazao yaliyochaguliwa kwa ajili ya chakula ni mtama, uwele, viazi vitamu na mikunde na mazao ya biashara ni alizeti, pamba, vitunguu na asali.

 

Wajumbe wa kikao hicho kwa kauli moja, wameazimia kuweka msisitizo wa kuzalisha mazao hayo na kwamba uhamasishaji ufanyike ili wakulima washiriki kikamilifu katika kuzalisha mazao hayo.

Aidha, wajumbe wa kikao hicho wamependekeza sheria ndogo ndogo  zitungwe katika kila halmashauri mkoani Singida, ili kuhakikisha kila kaya inakuwa na hekari walau tatu za mazao yanayostahimili ukame, ambayo ndiyo mkobozi kwa wakulima kuondokana na tatizo la uhaba wa chakula. Suala la matumizi mabaya ya chakula pia limejadiliwa katika kikao hicho na wakulima wametakiwa kutumia vizuri chakula wanachokipata.

 

Wajumbe wa kikao hicho pia wamejadili taarifa ya maendeleo ya elimu mkoani Singida, ambapo imeelezwa kuwa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012 mkoa wa Singida ni mabaya. Afisa elimu wa mkoa wa Singida Bi. Fatuma Kilimia amesema mkoa umeweza kufaulisha daraja la kwanza hadi la nne wanafunzi 2272, sawa na asilimia 23.8 kati ya wanafunzi 9,536 waliofanya mitihani hiyo.

 

Kutokana na takwimu hizo, amesema wanafunzi 7264 sawa na asilimia 76.2 walifeli kwa kupata daraja sifuri.

Thursday, March 21, 2013

MESSAGE ON THE INTERNATIONAL DAY OF FORESTS


 
the UN SECRETARY-GENERAL

--

MESSAGE ON THE INTERNATIONAL DAY OF FORESTS

21 March 2013

 

Forests are vital for our well-being.  They cover nearly a third of the globe and provide an invaluable variety of social, economic and environmental benefits.  Three-fourths of freshwater comes from forested catchment areas.  Forests stabilize slopes and prevent landslides; they protect coastal communities against tsunami and storm.  More than 3 billion people use wood for fuel; some 2 billion people depend on forests for sustenance and income, and 750 million live within them. 

 

By proclaiming the International Day of Forests, the United Nations has created a new platform to raise awareness about the importance of all types of forest ecosystems to sustainable development. 

 

Forests are often at the frontlines of competing demands.  Urbanization and the consumption needs of growing populations are linked to deforestation for large-scale agriculture and the extraction of valuable timber, oil and minerals.  Often the roads that provide infrastructure for these enterprises ease access for other forest users who can further exacerbate the rate of forest and biodiversity loss. 

 

Forests are also central to combating climate change.  They store more carbon than is in the atmosphere.  Deforestation and land-use changes account for 17 per cent of human-generated carbon dioxide emissions.  As weather patterns alter due to climate change, many forested areas are increasingly vulnerable.  This underlines the urgency of a global, inclusive, legally binding climate change agreement that will address greenhouse gas emissions and encourage the protection and sustainable management of forests.

 

Notwithstanding these immense challenges, there are encouraging signs.  The global rate of deforestation has decreased by almost 20 per cent in the past decade.  We need now to intensify efforts to protect forests, including by incorporating them into the post-2015 development agenda and the sustainable development goals. 

 

On this first International Day of Forests, I urge governments, businesses and all sectors of society to commit to reducing deforestation, preventing forest degradation, reducing poverty and promoting sustainable livelihoods for all forest-dependent peoples. 

 

Tuesday, March 19, 2013

TTCL YAAHIDI KUSHIRIKIANA STANDARD RADIO FM


VIONGOZI WA MAKAMPUNI YA STANDARD VOICE LIMITED NA TTCL MKOANI SINGIDA WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA BAADA YA KIKAO CHA KILICHOKUWA KIKIJADILI NAMNA TTCL INAVYOWEZA KUTUMIA RADIO KAMA NJIA MPYA YA MAWASILIANO BAINA YAKE NA WATEJA KATIKA KUBORESHA HUDUMA KWA WATEJA WA KAMPUNI HIYO KUBWA YA MAWASILIANAO YA SIMU TANZANIA



Wawili katikati ni Bw. James Japhet Daud (kushoto) mkurugenzi wa Standard Voice LTD na kulia aliyevaa koti Ni Bw. Mwambene Meneja wa TTCL mkoa wa Singida. picha na. Prosper Kwigize (meneja wa Standard Radio fm) 90.10 MHz SINGIDA

FUNDI MITAMBO WA STANDARD RADIO AMWAGIWA SIFA


UTANGAZAJI NI KAZI INAYOENDANA NA TASNIA YA UFUNDI, MAFUNDI WANA WAJIMBU MKUBWA WA KUANDA AU KUWEZESHA MITAMBO KUFANYA KAZI YA KUPITISHA SAUTI NA KUWA FURSA WATANGAZAJI KUPITISHA SAUTI ZAO KATIKA MITAMBO HUSIKA.

NI KWA SABABU HIYO, VIONGOZI WA DINI MKOANI SINGIDA, TEC NA BAKWATA PAMOJA NA JESHI LA PILISI WANAAMUA KUMPA PONGEZI FUNDI MKUU WA MITAMBO WA STANDARD RADIO KWA KUWEZESHA RADIO HIYO KUSIKIKA MKOA MZIMA WA SINGIDA NA MAENEO YA JIRANI

KATIKA PICHA KUSHOTO NI MOSES ANTHONY JOHN, FUNDI WA STANDARD RADIO AKITETA JAMBO NA VIONGOZI HAO.



DINI NA DOLA HAVIPASWI KUTENGANA KATIKA KUSAKA AMANI NA USALAMA WA TAIFA

Viongozi wa dini wanapoamua kushirikiana na viongozi wa vyombo vya dola ni dhahiri kuwa wameliona na kulitambua tatizo

hapo juu ni Askofu mteule wa jimbo la Bukoba na mlezi wa jimbo katoliki la Singida Askofu Lwoma (kushot) ACP Linus Sinzumwa kamanda wa polisi mkoa wa Singida na Shekhe Salum Ngaa wakiwa katika picha ya pamoja nje ya jengo la matangazo la Standard Radio FM baada ya kushiriki mjadala wa pamoja uliohusu kuwepo kwa dalili, hisia na matukio yanayoashiria udini nchini Tanzania na ushiriki wa vyombo vya dola katika kudhibiti usalama pale inapotokea dini kuanzisha chokochoko zinazotishia usalama wa taifa.

Viongozi wa kiislamu na kikristo mkoani Singida wameunda chombo cha pamoja kitakachoratibu masuala ya amani na usalama, chombo hicho kimepewa jina la kamati ya AMANI NA USALAMA MKONI SINGIDA, hii inaundwa na viongozi wa dini na vyombo vya dola.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida Linus Sinzumwa akisalimiana na mwandishi wa habari wa Standard Radio Bw. Boniface Mpagape ambaye pia ni Mhariri wa Habari mara tu baada ya kumalizika kwa mdahalo wa viongozi hao ulioandaliwa na mkuu wa kituo cha Matangazo cha Standard Radio Bw. Prosper Kwigize, kwa lengo la kujadili mstakabali wa amani ya Tanzania na chokochoko za kidini.

MSTAKABALI WA NISHATI TANZANIA-MDAHALO

Ajenda ya Maendeleo Baada-ya-2015 na Mustakabali wa Nishati Tunaoutaka kwa Wote
Tanzania, Norway na Umoja wa Mataifa washirikiana mjadala wa ajenda ya nishati
 
Dar es Salaam, Machi 18 Wakati mwaka 2015 unakaribia kwa kasi, bado kuna kazi kubwa ya kufanya kuharakisha kufikiwa kwa Malengo ya Milenia. Wakati huo huo, tunatakiwa tuanze kufikiria nini kitafuata baada ya mwaka 2015. Mjadala huu tayari umeshaanza, kama ilivyoonekana wakati wa “Rio+20”, na serikali katika miaka inayokuja zitajadili na kuamua ajenda ya maendeleo baada-ya-2015.
 
Katika kuchangia majadiliano haya, Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Nishati na Madini kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa na Ubalozi wa Norway nchini Tanzania wamewezesha, na kwa pamoja wanakuwa wenyeji wa mchakato wa mjadala wa wazi wa kanda Afrika ukihusisha makundi mbalimbali yenye maslahi ikiwamo serikali, asasi za kiraia, sekta binafsi, wasomi na vijana, kuelewa changamoto na fursa zao, na jinsi ya kuingiza masuala ya nishati kwenye ajenda ya maendeleo baada-ya-2015. Ripoti kutoka kwenye mashauriano haya itatoa mchango mzuri kwenye mkutano unaopangwa kufanyika katika ngazi ya kimataifa.
 
Nishati ni suala muhimu katika juhudi za kimataifa kushawishi mabadiliko ya dhana kuelekea kwenye kuondoa umaskini, shughuli za kiuchumi zinazojali mazingira na hatimaye maendeleo endelevu. Kwa namna mbalimbali, mjadala wa kimataifa kuhusu nishati na maendeleo endelevu tayari umeshaanza. Miaka mitano iliyopita imeshuhudia kuongezeka kwa shauku kuhusu masuala ya nishati, ikianza na tamko la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuutaja mwaka 2012 kama “Mwaka wa Kimataifa wa Nishati Endelevu kwa Wote”. Kwa kutambua umuhimu na uharaka wa changamoto za nishati, viongozi katika serikali, biashara na asasi za kiraia wanahitaji kujenga uelewa kimataifa juu ya umuhimu wa nishati kwa maendeleo endelevu.
 
Katika mchakato wa kuhusisha wadau kuhusu hayo yaliyoelezwa, mkutano wa majadiliamo umepangwa kufanyika tarehe 19 Machi 2013 kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Watoa mada  wakuu mbalimbali akiwemo Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa; Mkurugenzi wa Nishati, Mazingira na Mabadiliko ya Tabia Nchi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika na Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Norway wamealikwa. Mkutano huu utafunguliwa na Waziri wa Nishati na Madini Mheshimiwa Prof. Sospeter Muhongo.
 
Masuala muhimu yatakayojadiliwa wakati wa mkutano ni pamoja na : Upatikanaji wa Nishati kwa Wote; Kuongezeka kwa Ufanisi na matumizi endelevu ya  Nishati.
Wadau wote wa nishati wanakaribishwa katika mkutano huu.
 
Kwa Taarifa Zaidi Wasiliana na:                       
Mr Styden Rwebangila, Government stydenr@yahoo.com
Ms. Stella Vuzo, United Nations Information Officer at stella.vuzo@unic.org,    
Mr Geir Yngve Hermansen, Norwegian Embassy geir.yngve.hermansen@mfa.no
 

Tuesday, March 12, 2013

TAARIFA YA HABARI MARCH 12, 2013


Source: SR/Neema J.

Ed: BM

Date: March 12, 2013.

 
SINGIDA

 

Mtu mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa  baada ya gari walilokuwa wakisafiria  kupinduka  baada ya kutokea hitilafu za kiufundi  na kusababisha ajali hiyo katika  kijiji cha  kisaki  tarafa ya mungu maji mkoani singida.

 

Kamanda wa polisi mkoani Singida ACP Linus Sinzumwa amesema ajali hiyo imetokea jana majira ya saa nne usiku katika barabara ya Singida kwenda Dodoma na kutaja namba ya usajili ya gari hilo kuwa ni gari namba C 6017 aina ya Nissan presage.

 

Kamanda Sinzumwa amesema chanzo cha ajali hiyo  ni kutokana na rock  hand  na driving  shaft ya gari hilo kukatika hivyo kusababisha ajali na kumtaja aliyefariki kuwa ni Abubakari Bukungukize ambaye ni mfanyabiashara wa Rwanda,  na aliyepata ajali ni  Vidal Ruse ambaye ni raia wa Sweden

 

Pia amesema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya mkoa wa Singida na majeruhi bado anaendelea na matibabu na uchunguzi bado unaendelea kufanyika.

 

Amesema bado wanaendelea kuwasiliana na ndugu zao ili waje kuchua maiti na majeruhi huyo

 


Source: SR/

Ed: BM

Date: March 12, 2013.

 

KASULU

Katibu wa itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapinduzi CCM wilayani Kasulu Mkoani Kigoma Bw. Masud Kitowe ameuagiza uongozi wa kata ya shunguliba na kijiji cha malalo wilayani humo kuhakikisha mafundi waliopewa kazi ya kujenga nyumba ya mwalimu katika shule ya msingi malalo wanakamilisha ujenzi huo mara moja

 

Bw Kitowe ameyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha malalo wilayani kasulu baada ya kufanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata ya shunguliba sambamabamba na kufanya ukaguzi juu ya utekewlezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi.

 

Bw Kitowe amesema amepata taarifa kuwa mafundi waliopewa kazi ya kujenga nyumba hiyo wamesimama kuendelea na ujenzi kwa kile kinachodaiwa kuwa mafundi wamekwenda katika mashamba yao kulima. Amewaagiza viongozi hao kuhakikisha mafundi hao wanarejea na kumalizia ujenzi huo mara moja

 

Aidha Bw Kitowe amewataka viongozi hao kuhakikisha mafundi hao wanapatikana na kuendfelea na ujenzi wa nyumba hiyo na kama itashindikana basi mafundi hao warejeshe pesa walizopewa kwa ajili ya ujenzi huo na kuikabidhi kazi hiyo kwa mafundi wengine ili kukamilisha ujenzi wa nyumba hiyo ya mwalimu shuleni hapo


Source: SR/E. LYATUU

Ed: BM

Date: March 12, 2013.


SINGIDA

 

Wananchi Katika manispaa ya Singida wametakiwa kuwa  makini    na utupaji ovyo wa  taka  ili  kuweka   mji  safi  na  kuepukana   na  magonjwa  ya  mlipuko  mkoani   hapo

 

 

Bw. Seif  Swedy,  afisa  afya   na mazingira    wa   manispaa   amesema  hayo    wakati   akizungumza   na  standard    redio  ofisini  kwake.

 

 

Amesema  kuwa endapo wananchi wataonyesha  mwitikio kwa  kujituma kusafisha maeneo yao na kukusanya  taka  sehemu  moja,  hakutakuwa na  magonjwa ya   mlipuko kama  vile   kipindupindu    na   badala   yake mji  kuwa   safi na swala   la afya   kuwa   katika   usalama.

 

Hata hivyo  amesema chanzo  cha  taka  kuzagaa  ni kutokana   na  wananchi kutojali afya zao kutokana na hana  potofu  waliojiwekea  kwa kuamini suala la usafi linahusika na manispaa, hivyo  amewataka wananchi wawajibike  katika kuweka   mji  katika hali ya usafi.   

 

Bw  Seif  Swedy amewataka wananchi kuwa na mwamko wa  kujali mazingira kuwa katika hali  ya  usafi  na kila  mwananchi    kuwa mlinzi  wa mwenzake,  ili  kudhibiti tatizo la  utupaji   ovyo   wa  taka na kufuta dhana ya kutegemea manispaa   kuhusika  na  usafi   katika   mji  huo

 

Source: Tanzania Daima

Ed: BM

Date: March 12, 2013.

DAR ES SALAAM

Vituo vya televisheni vinavyomilikiwa na kampuni binafsi, viko hatarini kufungwa kutokana na mfumo wa matangazo wa digitali kuathiri upatikanaji wa matangazo.

Vituo vilivyopo kwenye hatari ya kufunga matangazo yao ni pamoja na ITV, Star TV, Clouds TV, DTV na vingine binafsi.

Taarifa za kufungwa kwa vituo hivyo, imetolewa jana na Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Nchini MOAT upande wa televisheni, wakati wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa MOAT, Bw. Reginald Mengi, amesema vituo hivyo viko hatarini kufungwa kwani idadi kubwa ya watumiaji wa televisheni imepungua kutokana na kukosa ving’amuzi na hivyo kuathiri upatikanaji wa matangazo.

Bw. Mengi amesema ili matangazo ya vituo vya televisheni yaendelee kupatikana, ameitaka serikali irejeshe matangazo ya analojia sambamba na digitali ili kuwapa nafasi watumiaji wa televisheni kujiandaa kuingia kwenye mfumo wa digitali.

Ameikosoa serikali kwa kuingiza matangazo ya mfumo wa digitali haraka bila kutoa muda wa kutosha kwa wananchi kujiandaa kwani haoni sababu ya Tanzania kuingia haraka kwenye mfumo huo.

Naye Mkurugenzi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, anayemiliki kituo cha televisheni cha Clouds, amesema nusu ya matangazo kutoka kwa wateja wao yameondolewa baada ya matangazo yao kutowafikia watu wengi.

Kwa upande wake, Samuel Nyala, Mkurugenzi wa Sahara Media Group wamiliki wa kituo cha Star TV, amesema baadhi ya mikoa iliyoanza kurusha matangazo ya digitali, wamekwama kwani hakukuwa na maandalizi wakati mitambo ya analogia inazimwa.


Source: SR/Beatrice

Ed: BM

Date: March 12, 2013.

SINGIDA

Watu watano wakazi wa manispaa ya Singida, wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi, wakikabiliwa na shtaka la kuvunja na kuiba katika jengo la kampuni ya vinywaji ya Bonite, eneo la Mwenge mjini Singida.

Akisoma kesi hiyo mwendesha mashtaka, Bw. Mussa Chemu mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi, Bi. Telsefia Tesha, washtakiwa hao wamekana mashtaka dhidi yao.

Imeelezwa kuwa February 18 mwaka huu, majira ya usiku maeneo ya Mwenge ulifanyika uvunjaji huo na mali yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni ishirini na tatu Mali ya kampuni ya Bonite. 

Washtakiwa hao watano ni walinzi wa kampuni hiyo, ambao ni Zabron Ibrahim mkazi wa Puma Singida, Kautusi Francis mkazi wa Unyamikumbi Singida, Kassim Peter mkazi wa Misinko Singida, wengine ni Ladislaus Masini mkazi wa kibaoni Singida na Musa Gambuna mkazi wa kibaoni Singida.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 26 mwezi huu itakapotajwa tena, na upelelezi bado unaendelea kufanyika wakati washtakiwa wamerudishwa rumande. 


Source: SR/Matinde Nestory

Ed: BM

Date: March 12, 2013.

                                          

 MWANZA

Meneja Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka katika jiji la Mwanza Bw. Robert Masunya amewataka wananchi kujitokeza katika maadhimisho ya siku ya maji yatakayofanyika wiki hii

Wito huo umetolewa mapema hii leo wakati radio standard ilipokuwa ikifanya mazungumzo ofisini kwake

Bw.Masunya amesema kuwa maadhimisho hayo yatafanyika march 16 mwaka huu katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza ambapo kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji ni march 22 mwaka huu.

Meneja Uhusiano huyo amesema kuwa kauli mbiu ya mwaka huu  katika siku ya maji ni MWAKA  WA  USHIRIKIANO  WA  MAJI  KIMATAIFA ambapo amewataka wananchi  kujitokeza katika maadhimisho hayo ambayo yanalenga katika kudumisha ushirikiano, upandaji miti katika vituo vya maji  pamoja na kutatua matatizo ya wananchi.