Thursday, May 2, 2013

BONANZA LA STANDARD RADIO MEI MOSI 2013- MATUKIO KATIKA PICHA

Timu ya soka ya Standard Radio katika picha ya pamoja kabla ya mechi kati yao na mashabiki na wapenzi wa radio hiyo ijulikanayo kama STANDARD RADIO SALAAM CLUB FC muda mfupi kabla ya kuanza kwa mpambano ambao hata hivyo hakukuwa na mbabe baada ya timu zote kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja, mpambano huo ulichezwa katika uwanja wa ufukwe wa Ziwa Kindai mjini SIngida
 
 
Meneja wa Standard Radio Bw. Prosper Kwigize akisikilliza maelekezo ya kocha muda mfupi kabla ya mechi kuanza, Kwigize kutoka winga ya kulia ndiye aliyetoa pasi iliyosababisha kupatikana kwa bao la kusawazisha kipindi cha pili, mbele aliyeshika nyonga ni mchezaji centre half Imani Msigwa



























Kikosi cha Standard Radio FC kikijipanga kuzuia mpira wa adhabu kutoka kwa wapinzani wake STANDARD salaam club FC, Mwenye jezi namba 13 mgongoni ni mwanaspoti wetu Cales Katemana na jezi namba 12 ni Abdul Bandola  mtayarishaji msaidizi wa kipindi cha Michezo kinachorushwa na standard radio kila siku saa moja na nusu jioni



























Abdul Bandola (kulia menye bukta ya njano) star wa Standard Radio fc akichapa mwendo kufunga bao la ushindi, hata hivyo walinda mlango wa Salaam Club FC walifanikiwa kuzuia mashambulizi.

Meneja wa Standard Radio akiongoza kikosi cha mashabikii na watangazaji kuelekea uwanjani tayari kwa mtifuano wa Bonanza la Standard radio na Mei Mosi, Standard Radio Imeahidi kuendesha matamasha mbalimbali pamoja na mashindano ya soka kwa wanaume na wanawake kama sehemu ya kuitangaza Radio hiyo, Hivi karibuni lilifanyika tamasha kubwa na zuri wilayani Ikungi na inatarajiwa kufanyika tena mjini Singida na Iramba kabla ya kuenlekea Igunga na Nzega mkoani Taboba na baadaye matamasha hayo yatafanyika katika wilaya za Hanang na Mbulu mkoani Manyara

Bw. Boniface Mpagape (mwenye koti) ambaye ni Mhariri wa Standard Radio ambaye ni Mhariri akiongoza kikosi cha pili cha soka kutoka SR FM kuelekea uwanjani muda mfupi kabla ya mechi hiyo kuanza, Mpagape a.k.a Furgason) ndiye Kocha mchezaji wa timu ya soka ya Standard Radio

1 comment:

Unknown said...

thanks alot Manager of Standard Radio for the occassion held on Mei Mos, Keep it continuosly