Monday, July 30, 2012

TAKWIMU STANDARD ZA MTANDAONI


YALIYOJILI MTANDAONI


MWEZI MMOJA TU TANGU BLOG YA STANDARD RADIO KUPEPERUSHWA MTANDAONI MAMIA YA WASOMAJI WAMEUTEMBELEA
Kushoto mwa ukurasa huu ni taarifa za walioutembelea mtandao wa Standard Radio Fm kupitia katika Blog yetu
Hii inaashiria kuwa tayari tnatambulika duniani kote na tunakubalika, pamoja na takwimu hizo, tumepokea maoni mengi sana kuhusu BLOG hii pamoja na maoni ya jumla kuhusu Radio yetu, katika taarifa zetu zijazo tutabandika maoni hayo
TANGAZA NA STANDARD RADIO UJULIKANE DUNIANI


WASOMAJI WA MTANDAO NA NCHI ZAO
· USA————63
· TANZANIA ———191
· RUSSIA————4
· GERMAN———1


Tuesday, July 24, 2012

NAFASI ZA KAZI

STANDARD RADIO FM 90.1 FM

Ambayo iko mkoani Singida katikati mwa Tanzania inawatangazia nafadi za kazi mbalimbali kama ifuatavyo

1. Uandishi wa habari na utangazaji------------nafasi 5
2. Afisa masoko na mahusiano------------Nafasi 1
3. Fundi Mitambo--------------------nafasi 1
4. Fundi wa Computer---------------Nafasi 1
5. Dreva-----------------------Nafasi 1
6. Mhudumu wa ofisi..............Nafasi 1

SIFA ZA MWOMBAJI
Mwombaji wa nafasi yoyote kati ya hizo unapaswa kuwa na sifa zifuatazo
1. Elimu ya Msingi, Sekondari, chuo
2. Uwe umefanya kazi unayoiomba kwa angalau miaka miwili mfululizo
3. Dreva awe na leseni class A, B, D au C na awe na ujuzi wa Ufundi
4. Mwandishi wa Habari au Mtangazaji awe na cheti cha chuo kinachotambuliwa na NACTE na awe na uzoefu, sauti nzuri, na mwenye uwezo wa kuandika miradi (project writeup) au Program Proposal, awe na nakala ya habari iliyochapishwa au kutangazwa na chombochochote katika kipindi cha miezi 12 kabla ya maombi
5. Uwe na uwezo wa kuzungumza Kiswahili fasaha, na kiingereza, kwa anayejua kifaransa ana fursa zaidi

NB: fundi Mitambo atakayekuwa na ujuzi wa computa IT pamoja na fani ya Udereva na wenye leseni atapata fursa ya kufikiriwa zaidi

MAWASILIANO

BARUA ZA MAOMBI ZITUMWE KWA

Standard Radio Fm
P.O. Box 62
Singida
Tanzania
e-mail  srfm2011@gmail.com au standardradio2011@hotmail.com
Blog yetu. www.standardradiofm.blogspot.com

Mwisho wa kutuma maombi ni 10/08/2012

Monday, July 9, 2012

TACAIDS YATOA MAFUNZO KWA WANAHABARI

WAANDISHI WA HABARI licha ya kutumika kuhabarisha, kuelimisha na kuburudika, wanalo jukumu kubwa kwao wao wenyewe kujifunza na kuwa na elimu ya yale ambayo wao wanataka kupitia vyombi vyao wayajue. hivi karibuni Tacaids ILITOA MAFUNZO kwa waandishi wa habri wa vyombo mbalimbali vya habari hususani radio za kijamii ili kuwawezesha kutimiza wajibu wao kwa wanaovisikiliza vyombo yao.

Pamoja na majukumu megine STANDARD RADIO FM, inakusudia kuwajengea uwezo wanahabari wake watakaopata ajra kujifunza kwa kina juu ya maadiliko na mbinu za kumfikia msikilizaji kadiri ya wakati

HILO NDILO LENGO LETU

Friday, July 6, 2012

VYOMBO VYA HABARI NA UKIMWI

Tume ya taifa ya kudhibiti UKIMWI Tanzania TACAIDS imetambua kuwa wanaadhisi wa habari, watangazaji na vyombo vyao wana mchango mkubwa katika kuelimisha jamii kuhusu HIV/AIDS na hivyo kutoa mafunzo ya utambuzi wa jinsia katika kuandika, kutangaza na kutafiti masuala ya kijamii yanayohusu JINSIA na UKIMWI

Standard Radio imeshiriki kikamilifu kwa kuwakilishwa na Ndg Prosper Kwigize

Mafunzo yamefanyika jijini Dar es salaam July 2012

Wednesday, July 4, 2012

MAWASILIANAO YANA MAANA KUBWA

        
Mawasilianao ndiyo njia ya kujenga maafikiano na mahusiano, sisi SR fm tunaamini kuwa mawasiliano ndiyo njia pekee ya kufikia mafanikio tunayoyatarajia, tunaamini wewe ni mdau mhiu wa mawasiliano , Tunakualika uwasialiane nasi kwa lolote, yaweza kuwa maswali au hata maoni kuhusu Blog yetu au kuhusu Radio pia. hapa chini ni anuani yetu
KARIBU        
Standard Radio Fm
P.O. Box 62,  SINGIDA, TANZANIA
MANAGING DIRECTOR–  0787 592 056
PROJECT MANAGER— 0786 200 518
E-MAIL. standardradio2011@hotmail.com
SRfm2011@gmail.com

Tuesday, July 3, 2012

TUSOME JAPO KWA SHIDA

MWANZO NI MGUMU JAMA-  HII NI SHULEYA SEKONDARI SUMA ENGI KARET LONGIDO ARUSHA
ukiangalia mazingira haya huwezi kuamini kuwa kuna elimu hapa, nina hakika watoto kutoka Bukoba, Kigoma na Moshi ambako leo kila kata kuna shule huwezi kuamini kuwa Mapadre hawa wa shirika la Roho mtakatifu wameamua kuja Kuishi katika jangwa hili lenye miti ya miiba ili kusaidia watoto wa kimasai kupata elimu, hiii ni kazi nzito yenye uhitaji mkubwa wa wito

Tusome japo kwa shida, Watoto anaosoma katika mazingira haya nina hakika wengine watakuwa watangazaji ambao watapiga kelele dhidi ya mila potofu zinazong'ang'aniwa na baadhi ya makabila na hasa wa masai wasiotaka kusomesha watoto

ELIMU NA MAWASILIANO DIRA YA MAENDELEO

Padre Karumuna, mkuu wa shule ya sekondari SUMA Engikaret Arusha akikagua mazingira ya shule hiyo changa iliyoko kijijini kabisa mahala ambapo wawekezaji wengine katika elimu hawafikirii kabisa kwenda kuibua changamoto na mateso yanayowakabiri watoto wa kimasai,

WAMASAI ENGI KARET WAAMUA KUSOMESHA WATOTO

Sirika la kimisioni la ROHO MTAKATIFU la kanisa Katoliki limejikita katika vijiji ambavyo ni makazi wa WAMASAI huko mkoani Arusha katika wilaya ya LONGIDO ambapo kupitia katika shule ya sekondari SUMA Egi Karet zaidi ya watoto 100 wa kabila la wamasai wanapatiwa elimu

Hata hivyo zipo changamoto nyingi sana za kimiila na utamaduni wa wamasai kutopenda kuwasomesha watoto wao ili wabaki kuwa wachungaji wa mifugo kwa watoto wa kiume na watoto wa kike waolewe ili kuongeza idadi ya mifugo
Pongezi za pekee ziwaendee mapadre wa Roho mtakatifu EGI KARET LONGIDO, Padre Karumuna na Padre Chundu waliompokea mkurugenzi wa Standard Radio aliyetembelea kijiji cha Eng karet na kushuhudia watoto wa kimasai wakisoma

watoto wote walitamani kuwa wanahabari mara tu waliporekodiwa na kufundisha juu ya mfumo wa utayarishaji wa habari na vipindi vya radio, Sina shaka Padre Karumuna atawawezesha siku moja waitembelee Standard Radio mjini Singida kwa ajili ya ziara ya mafunzo, kwa njia hii tutaibua vipaji vingi kwa watoto walioko sekondari.

"DAFTARI ULILONALO DAWATINI NA UBAO WA KUANDIKIA DARASANI NDIYO NJIA YA MAISHA YAKO MWANAFUNZI"

MKUU WA MKOA SINGIDA, AKIRI MAWASILIANO NI MUHIMU

Mkuu wa mkoa wa Singida Pasekoo Kone, akihutubia mkutano wa wadau wa matumizi ya mawasiliano mkoani Singida, ambapo pamoja na mambo mengine katika hotuba yake amekiri kuwa, vyombo vya mawasiliano hususani Radio, Simu na Runinga katika kukuza uchumi katika sekta ya kilimo na masoko.

Moja ya malengo ya standard radio fm ni kuwawezesha wakulima na wajasiliamali wa kati na wa juu, kujua nini kilichopo katika anga la uchumi na wapi wanaweza kupata soko la bidhaa zao hasa mazao ya mashambani na ya viwanda vidogo vidogo.

Ni dhahiri kuwa, Tanzania sehemu yake kubwa ya uchumi hutegemea Kilimo na viwanda vidogo vodogo,, pamoja na utegemezi huo, Bado watanzania hawajapata elimu ya kujua fursa za masoko ya bidhaa wanazozalisha, hivyo basi STANDARD RADIO FM, inakuwa SIngida ili kuonesha njia ya kuelekea uchumi unaotokana na kila mtu kutimiza wajibu wake hasa baada ya kuzijua fursa ziliopo

HII ndiyo Kazi yetu Standard Radio Fm

MKUU WA MKOA SINGIDA AFURAHIA UJIO WA SRANDARD RADIO FM

MKUU WA MKOA SINGIDA APONGEZA APONGEZA UJIO WA STANDARD RADIO
Mkuu wa mkoa wa Singida amepongeza uamzi wa kampuni ya Standard Voice LTD wa kuja kuwekeza katika mawasiliano mkoani Singida hasa kwa kuanzaisha kituo cha radio ya Standard Radio FM na kukiri kuwa ni mapinduzi ya maendeleo kwa mkoa.
Akiongea na meneja wa Standard Radio fm Ndg Prosper Kwigize jana mjini Singida wakati wa semina ya mamlaka ya mawasiliano Tanzania TRCA, mkuu hyo wa mkoa Dr. Paseko Kone amekiri kuwa uanzishwaji wa Radio itakayorusha matangazo yake kutoka Singida ndio njia pekee ya kuinua uchumi wa wananchi pamoja na kupanua wigo wa mawasiliano.
Aidha katika maelezo yake mkuu wa mkoa wa Singida Dr. Parseko Kone amepongeza vyombo vya mawasiliano nchini kwa kuwawezesha wakulima mkoani humo kupata masoko ya mazao kwa njia rahisi na hivyo kukuza uchumi wa kaya zao
Dr. Kone amebainisha hayo jana (jumanne) mkoani Singida wakati akifungua warsha ya wadau wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA iliyokuwa ikijadili ukuaji wa sekta ya mawasilano Tanzania
Alibainisha kuwa, katika kipindi kifupi cha ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano husani uwepo wa simu vijijini, matangazo ya Radio na Runinga, wakulima wameweza kujua wapi kuna soko la mazao yao
“kila ninapokwenda vijijini wananchi hususani wakulima wa vitunguu wananiambia wazi kuwa sasa soko la vitunguu liko wazi na hawahangaiki sana kuvisafirisha kwenda sokoni balii wateja kuwafuata wenyewe, na hata wanaposafirisha wanakwenda wakijua bei hivyo hawawezi kuibiwa au kuuza kwa hasara” alisema Dr. Kone
Hata hivyo pamoja na pongezi hizo, mkuu huyo wa mkoa wa Singida ameonya kuwepo kwa matumizi mabaya ya mawasiliano ambayo yamekuwa yakipotosha jamii na kupoteza utamaduni na maadili ya jamii
Alieleza kuwa, matangazo mengi hasa katika vyombo vya matangazo hayazingatii maadili na hivyo huchochea kuporomoka kwa maadili na kupoteza uzalendo miongoni mwa watanzania
“Mimi ninashangaa, unaweza ukaona kipindi katika Runinga kikionesha mambo ambayo kwa hakika ni potofu kabila, ni kinyume cha maadili ya mtanzania, sasa najiuliza ni nani anaruhusu matangazo au vipindi hivyo kuoneshwa au kutangazwa? Taifa letu wanataka lielekee wapi jamani” alieleza Kone kwa masikitiko makubwa.
Wakati huo huo, mkuu huo wa mkoa wa Singida ametumia fursa hiyo kutoa onyo kwa watu ambao wameanza kupotosha dhana nzima ya sensa ya watu na makazi na kueleza kuwa makampuni ya mawasiliano zikiwemo radio na runinga zitumie vyombo vyao kuhamasisha jamii kujitokeza kuhesabiwa
Dr. kone amebainisha kuwa yapo makundi ya watu ambayo yanaeneza uvumi kuwa serikali anataka kuwahesabu watu ili kupandisha kodii na kuanzisha kodi mpya hasa za mifugo na kwamba hayo ni maneno ya kupotosha jamii
Warsha ya wadau wa mawasiliano iliandaliwa na mamlaka ya mawasiliano Tanzania TRCRA kwa lengo la kuwawesha wadau kutambua wajibu na haki ya matumizi ya vyombo vya mawasiliano kwa ajili ya maendeleo ya teknolojia na maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Mwisho



VETA YASHIRIKI KAZI NA MAFUNZO


Wanafunzi wa chuo cha mafunzo ya ufundi stadi VETA SINGIDA, wakishiriki mafunzo na kazi wakati Standard radio ikijengwa mjini Singida mita chache kutoka kilipo chuo cha VETA

Tunampongeza Mwl Lyimo kwa kuleta vijana wake kwenye mafunzo, tunaimani kuwa watakuwa mafundi wazuri kwa ujenzi wa taifa letu

KAZI NA MAFUNZO

katika picha, wanafunzi wa chuo cha mafunzo stadi VETA Singida wakiwa katika moja ya mafunzo wakati wa ujenzi wa mnara wa Standard Radio fm, mwenye koti la rangi ya Bluu ni mwalimu LYIMO kutoka kitengo cha ufundi vyuma chuoni VETA

Tunachukua fursa hii, kumshukuru sana Mwl Lyimo kwa ushirikiano wake wa hali na mali wakati wa ujenzi wa mnara huo

aidha tunakishukuru chuo cha VETA Singida kwa kutupa ushirikiano wa kiufundi, tuna imani kuwa ushirikiano huu utaendelea daima

DIRA NA MTAZAMO WA STANDARD RADIO


VISSION

To be the best Radio in Tanzania which will provide comprehensible, balanced and accurate news at the local, regional, national and international levels”


MISSION


To be the bridge and centre that will empower its listeners to articulate their concerns and to mobilize them for community economic development via small, medium and large entrepreneurship from the village up to the National level”


Through the Standard Radio Vision and mission, The radio will provides formal educational programs for primary schools students, and on-going education programs in topics like health, nutrition, agriculture, environment, law, human rights and role of civil society in community development

JENGO LA MATANGAZO

HII NI NYUMBA YA MATANGAZO
Nyumba hii ndio mahali ambapo matangazo yote ya Standard Radio yatafanyika, jengo hili la STUDIO liko eneo la GENERY mjini Singida karibu na mradi mpya wa maji Singida

ROMA HAIKUJENGWA KWA SIKU MOJA

HAPO PICHANI---Fundi wa Mnara ndg MBONDE kutoka Dar es salaam, akikwea mnara wakati wa ujenzi, walioko chini ni Msimamizi wa mradi Bw. Prosper Kwigize (mwenye suti) Mwalimu LYIMO kutoka VETA Singida ambaye licha ya kuleta wanafunzi wa fani ya vyuma alishiriki kikamilifu kutoa ushauri wa kiufundi wakati wa ujenzi wa Mnara huo, na anayevuta kamba ni mfundi msaidizi wa mnara Bw. Masoud naye kutoka DSM

RADIO YETU, JINA NA MAANA


NAME OF THE RADIO

The Radio is known as STANDARD RADIO FM. We will be available at 90.1 fm in Singida region. We have also plan  to be available country wide in future.


SR FM, we expect that the existence of this radio will be very much informative to the audience about trade and industry development, politics, relationship between the local communities and central communities, culture conservation, health and environmental issues. Standard Radio also meant to make its broadcasting to be very standard by professionalism

This Radio project is meant to help people to know what is taking place in the locality, what are the projects hosted by the NGOs and individuals operating in the surrounding of their locality, and inform the public in general.

The project would also alleviate the problem of lack of information for people who have been waiting for news which aired by other Radio stations and newspapers coming from out, which don’t even include local stories from Singida villages, hence   people are lagging behind on the right of freedom of expression

The project also aims at delivering awareness of HIV/AIDS to youths who are not informed enough, we are devoted also to inform our community about the real economic situation around them. It also aims at encouraging farmers, peasant and businessman to use media as a tool to meet success.

JENGO LA MITAMBO

Hili ni moja ya majengo ya Standard radio kama linavyoona kabla ya kukamilika kwake, jengo hili ni la kisasa kabisa na limejengwa kwa kuzingatia mahitaji ya mitabo ya Digital

PICHA YA MNARA BAADA YA UJENZI

Hili ndilo eneo la urushaji wa matangazo ya Standard Radio Fm 90.1 Mjini Singida, matangazo yataanza kuruka hewani hivi karibuni, Kwa wakazi wa mkoa wa Singida huu ni ukombozi mkubwa na wa pekee kwani tangu uhuru hakuna radio inayorusha matangazo yake kutoka Mjini Singida.

Hata hivyo sisi SR Fm tunatoa pongezi za dhati kwa kabisa kwa wakazi wa mkoa wa Singida ambao mmeipokea nia yetu kwa shangwe, tunayo hakika kuwa mtashirikiana nasi pia katika kutekeleza malengo yetu

mitambo hii ipo eneo la VETA Singida kiasi cha mita 600 nyuma ya majengo au eneo la VETA, hata hivyo matangazo yatafanyika eneo la GENERY ambako studio zimejengwa


STANDARD RADIO ITAFANYA NINI CHA PEKEE


We are going to work hand in hand with institutions in and out of Tanzania Mainland and Zanzibar to promote community participatory development, transparence, good governance, health issues, environmental issues and community integrations through reporting different news and radio programs which will have all elements of Educating, Informing and Entertaining.


Both we know that, Lack of communication and media organizations in Central and western Region of Tanzania is a barrier to development. This is due to the absence of information, people from the regions and their neighbours are ignoring what their rights are, what their responsibilities are, and what is the importance of media in the promotion of development through increase of daily income generating activities, democracy, good governance, fight against corruption, HIV/AIDS, Malaria and the like. 

NI NANI MMLIKI WA STANDARD RADIO?

The Standard Voice Limited who is Standard Radio fm owner is a registered company in the United Republic of Tanzania with incorporation registration number 81651 of 2011
 
The Standard Voice LTD is a company devoted to help the Tanzania community to meet their development goals via   Radio and Television Broadcasting activities in United Republic of Tanzania at large stating with central and western zone of Tanzania

INTRODUCTION
 
As we know that, the media have power and big contribution to the development of any country, so after, the Radio that we are expected to establish very soon will be a forum of media practitioners who’s devoted to discuss collectively issues pertaining to media practitioners and promotes obedience to ethical and professional standards, and we shall provide community and development forums and facilitate dissemination of information in the United Republic of Tanzania.

LENGO LETU


When we are talking about  the Voice of the Voiceless we mean that, people are living in different challenges , and  to stop the silent is the way to solve and overcome those challenges, so our objectives will stick on the community agenda

Main Objective Of Standard Radio FM.

To work parallel with the millennium goals through information sharing and promoting community participation in decision making into development projects.
Either the objectives shown below in detail is our major target of this Radio in Singida region.

KARIBU

STANDARD RADIO FM

THE VOICE OF THE VOICELESS

SAUTI YA WASIO SIKIKA