Friday, August 31, 2012

SINGIDA PRESS CLUB YAPEWA SOMO


Na Evarista Lucas

Singida

 

 

Mkuu  wa wilaya ya Iramba  Bwana Yahya   Nawanda; amewaasa viongozi na wanachama wa Klabu ya waandishi wa habari Singida(SINGPRESS  kuyafuata yale waliyoafikiana katika mkutano na kuhakikisha kuwa hawaendi kinyume na mabadiliko hayo.

Akihutubia wanachama hao katika mkutano wao wa marekebisho ya katiba ya SINGPRESS uliofanika katika kijiji cha Kiomboi wilaya ya Iramba mkoani Singida; Nawanda aliwawataka wanachama hao kuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa kufuata maadili ya kazi yao.

“Siku hizi tasnia ya uandishi wa habari imekuwa inaingiliwa sana na watu na watu wasiokuwa na maadili  ambao ndio wanaofanya kazi hii na heshima mbele ya jamii, kwani uandishi ni maadili.” Alisisitiza Nawanda.

 

Kwa upande mwingine Nawanda aliwataka wanachama hao kuepukana na ushabiki wa kisiasa ili waweze kufanya kazi yao kwa ufanisi zaidi na kwa kuzingatia maadili ya kazi yao.  “Baadhi yenu mmekuwa wanasiasa tena wa wazi wazi. Mnafanya kazi ya  viongozi wa siasa. Mimi nawaasa mfuate maadili ya uandishi wa habari na kuachana na siasa.” Nawanda.

           

Licha  ya hayo  Nawanda aliwaomba wanachama hao kuandika pia mambo mazuri ambayo yamefanyika hapa mkoani ikiwemo ujenzi wa hospitali ya kisasa ya rufaa, barabara za lami na makazi bora.

 

“Tutawapa ushirikiano mkubwa waandishi wa habari kwani nyie ni watu muhimu kuhabarisha Watanzania kile tunachokifanya katika maendeleo ya mkoa wetu. Wasaidieni kuandika makundi maalumu kama   vile walemavu, changamoto zao na ustawi wao kwa ujumla na sio kujikita kwenye siasa tu. Sasa Tanzania tunajua mwandishi bora ni yule anayejikita kwenye siasa tu.”  Nawanda

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa SINGPRESS Bwana Seif Takaza alimshukuru mkuu huyo wa wilaya  kwa kuitikia wito wa kuwa mgeni wa heshima katika mkutano wao na pia kwa kuwapatia ukumbi uliowawezesha kuikamilisha kazi hiyo muhimu kwa maendeleo ya Klabu.

 

 “Hii ni awamu ya pili kwa waandishi wa habari kufika katika wilaya ya Iramba  awmu ya kwanza ilikuwa ni Mei 3 mwaka huu siku ya uhuru wa vyuombo vya habari ambapo tulikwenda kwa Wahadzabe na kutoa msaada wa chakula na vifaa vya shule. Leo tena awamu ya pili tunafanya mkutano huu hapa.

 

 Katika mkutano huo uliojumuisha wanachama kumi na saba (17) wa SINGPRESS wanachama walipata fursa ya kuipitia kwa umakini katiba hiyo na baadhi ya vipengele vilivyoongezeka katika katiba hiyo.”

Tuesday, August 28, 2012

MCT YAWANOA WANAHABARI KIGOMA KUHUSU TAMKO LA DSM

Waandishi wa habari mkoani Kigoma wakiwa katika picha ya pamoja na mkuu wa wilaya ya Kigoma Bw. ramadhan Maneno pamoja na wakufunzi kutoka MCT Bw. Deodatus Balile mhariri mtendaji wa gazeti la JAMHURI na Bi. Rose Mwalongo kutoka tume ya haki za binadamu na utawala bora na pia mwandishi wa gazeti la Guardian

Baraza la habari Tanzania linatoa mafunzo ya maadili na kulitangaza azimio la Dar es salaam kuhusu uhuru wa uhariri na uwajibikaji wa vyombo vya habari nchini Tanzania

Tama tamko la Dar es salaam litazingatiwa ni dhahiri kuwa kazi ya uandishi wa habari itakuwa rahisi na yenye tija kwa taifa la Tanzania

Tidha maadili ni jambo la muhimu ili kufanikisha utekelezwaji wa tamko hilo

Monday, August 27, 2012

ARCADO NTAGAZWA WAZIRI WA ZAMANI NA KAULI ZA KUTATANISHA


 

Arcado Denis Ntagazwa ni mmoja wa wasomi wa enzi hizo ambaye akitokea kijiji cha KIzazi wilayani Kibondo mkoani Kigoma alifanikiwa kushika nyadhifa nyingi ikiwemoo ubunge na uwaziri kwa nyakati tofauti tangu wakati wa Rais wa kwanza wa Tanzania hayati baba wa taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere

Ntagazwa ambaye amewahi kujinadi kama mbunge wa kudumu wa jimbo la Muhambwe aliangushwa na mwana usalama wa Ikulu Felix Ntibenda katika kinyang’anyiro cha Ubunge katika kura za maoni ndani ya CCM

Haikuwa jambo jepesi kumng’oa Ntagazwa kwani alikuwa amejizatiti vilivyo kwa kuwaweka sawa vijana, wanawake na wazee waliokuwa wamelishwa yamini kwa Khanga, Baiskeli na simu za mkononi alizowagawia kuwashawishi wamwamini kuwa ndiye anayefaa kuwa mbunge kwa miaka mingine 5 atimize miaka 30 ya ubunge

Leo Ntagazwa ni kamanda wa CHADEMA amekuwa akizunguka huku na kule kukinanga chama chake cha zamani CCM akiwatuhumu kuwa nii vinala wa Rushwa na wanadidimiza maendeleo

Ntagazwa hakukurupuka kwenda CHADEMA, kutokana na umakini na ufahamu wake alijipa muda wa kutafakari tangu mwaka 2005 hadi 2010 alipojaribu tena kugombea katika kura za maoni za CCM na kushindwa

Je?  anapopambana leo na CCM kwa tuhuma za RUSHWA ni dhamira ya dhati au HASIRA ZA KUUKOSA UBUNGE ndani ya CCM na hata huko chadema alikokwenda baadaye

Wanaharakati hasa vijana tunapaswa kujiridhisha na DHAMIRA ya NTAGAZWA na tujiulize pia kama yeye hakuwa mtoa rushwa kabla ya kuhujumiwa na wapiga kura waliokula vya kwake na kasha kumtosa katika karatasi za kura

Hizi siasa za watanzania wanaokuwa watakatifu mara wanapokosa nafasi CCM na kuhamia upinzani huku wakituaminisha kuwa wao ni wema na wanayajua madhambi ya zamani nadhani ni busara kama wakitanguliza kuomba radhi kwa maovu waliyafanya kabla ya kututangazia utakatifu wao baada ya kuhama CCM

Huo ndio uungwana na sisi tutawaamini

 

Haya ni Maoni yangu ninakaribisha mjadala katika hili

0764243377

MGOGORO WA MPAKA KATI YA TANZANIA NA MALAWI HALI TETE

Na. Prosper Kwigize

Baada ya mazungumzo kati ya Malawi na Tanzania kuhusu mgogoro wa mpaka katika Ziwa Nyasa kugonga mwamba, Tanzania imesema mazungumzo mengine yatafanyika tarehe 10 mwezi ujao kujaribu tena kutatua mzozo uliopo.
     
Katika mazungumzo yaliofanyika nchini Malawi mjini Mzuzu, Malawi ilitaka mzozo huo utatuliwe katika mahakama ya kimataifa ya ICJ.

Kwa upande wake Tanzania imepinga suaa hilo kutatuliwa na mahakama ya kimataifa badala yake kuwepo na mazungumzo zaidi

Hata hivyo serikali ya tanzania imeendelea na msimamo wake wa kupiga marufuku shughuli za utafiti wa mafuta zinazoendeshwa na Malawi

Hofu bado imetanda juu ya uwezekano mkubwa wa kuibuka kwa vita kali ya kugombania mpaka kama ilivyokuwa kwa Idd Amin Dada mwaka 1978

Nchi ya Malawi imelimega ziwa lote na kulifanya kuwa ndilo mpaka wa nchi zetu lakini haikufanya hivyo kwa upande wa Msumbiji ambao wao wanagawana ziwa hilo katikati

inakuwaje tanzania ihujumiwe kuwa ziwa lote ni la malawi lakini haifanyi hivyo kwa Mozambique?

angalia ramani hizi

 
Hii ni ramani inayoonesha mipaka ya Tanzania na nchi jirani kama ilivyochorwa tangu mwaka 1913, eneo la Ziwa Nyasa ambalo leo Malawi wanaliita Ziwa Malawi mpaka wa Tanzania na Malawi uko katikati ya ziwa, lakini malawi walibadili mpaka huo
 
 Ramani hii inaonesha sehemu ya ziwa Nyansa kama ilivyobadilishwa na Malawi miaka ya 1964 baada ya uhuru wa Taifa lao, eneo la ziwa linaiondoa Tanzania katika umiliki wa sehemu wa Ziwa hilo lakini ukitazama kwa chini eneo la Mozambique kitendo hicho hakikufanyika, wao wanagawana ziwa hilo katikati, Je ni nini hoja ya Malawi kwa Tanzania?
 
let us discuss

 

WAANDISHI WA HABARI MSIGEUZWE KUWA MABANGO


Mhariri mtendaji wa gazeti la JAMHURI Bw. Deodatus Balile amebainisha kutofurahishwa na tabia ya ngwaandishi wengi nchini kugeuzwa kuwa mabango ya makampuni na taasisi mbalimbali kwa kuvaa mavazi hususani fulana (tshirt) zenye matangazo

Balile amesema hayo mjini Kigoma wakati wa mafunzo ya maadili kwa waandishi wa habari mkoani humo sambamba na kufafanua azimio la Dar es salaam juu ya UHURU WA UHARIRI NA UWAJIBIKAJI yanayosimamiwa na Barala la Habari Tanzania MCT

Ameeleza kuwa maeneo mengi hususani mikoani waandishi wa habari wengi wamekuwa wakivaa kila e matangazo ya makampuni Fulani, jambo ambalo tafsri yake ni kwamba habari nyingi zinazoandikwa na waandishi hao ni zile zilizogharimiwa na mashirika, kampuni au taasisi iliyomgwia fulana au kofia.

“jamani vaeni mavani yenu tena yawe ya heshima, si kuvaa nguo za kupewa, kwani ninyi hamuwezi kujinunulia nguo? Hta hivyo nawapongza Kigoma hamna tabia hiyo ya kuguzwa kuwa mabango ya makampuni na mashirika kwa kuvaa mavazi yao” alisema Balileoni
Tanzania ni miongoni mwa nchi chini ya jangwa la sahara ambazo waandishi wake wa habari wanaishi kwa kipato cha chini sana kutokana na wamiliki wa vyombo vya habari kutowapa mikataba na pia kuwalipa kiwango kidogo cha mishahara au posho za kazi zao
kwa waandishi wa mikoani hasa wanaoandika habari za magazeti, wengi wao hawapati malipo kutoka kwa vyobo vyao na hivyo maisha yao huyaendesha kwa kutegemea posho kutoka kwa wadau wa habari, mashirika na taasisi mbalimbali za serikali, pindi wanapokuwa na jambo la kuandikwa au kutangazwa na vyombo vya habari hulazimika kutoa chochote (mshiko) ili habari zao ziandikwe
Jambo hili linachangia sana kuporomoka kwa maadili ya uandishi wa habari na vyobo vya habari.

MANYONI WAJITOKEZA KUANDIKISHWA-SENSA


 
Mkuu wa wilaya ya Manyoni mkoani Singida Bibi Fatuma Toufiq akitembelea moja ya kaya wakati za zoezi la sensa
Doris Meghji Jumatatu

Manyoni – Singida

Zoezi la sensa ya watu na makazi wilayani Manyoni linaendelea vizuri licha ya changamoto mbali mbali zilizojotokeza kwenye utekelezaji wa zoezi hilo katika baadhi ya vitongoji na vijiji juu ya suala la mipaka kati wilaya ya Uyui, Bahi,Sikonge na Manyoni

Mkuu wa wilaya ya Manyoni Bi Fatuma Toufiq ametoa taarifa hiyo wilayani humo jana mara baada ya kutembelea baadhi ya maeneo na kujua hali ya zoezi hilo limekwendaje

Bi Toufiq amesema kuhusu suala la mipaka katika vijiji vilivyoko mpakani kati ya wilaya yake na wilaya za Uyui,Bahi na Ikungu limetatuliwa kwa vijiji hivyo kuhesabiwa kuwa viko manyoni kutokana na ramani za kuhesabia maeneo (EA) zinavyoonyesha kwa makarani wa sensa ya watu na makazi wilayani humo

Aidha amesema katika wilaya yake wananchi wengi wameitikia zeozi hilo kwa kutoa ushrikiano kwa makarani wa sensa ya watu na makazi wa madodoso yote kwa kutoa taarifa sahihi kwa makarani huku akiwataka wananchi kutohujumu zoezhi hilo kwa kutoa ushrikiano kwa makarani wa sensa

Amesema “Ni kaya mmoja nilivyopewa taarifa kuna mtu alikataa kuhesabiwa akidai yeye ni muislam,lakini baada ya kuelimishwa na karani wetu alikubali kuhesabiwa kwa hiyo mwandishi hilo ni kaya moja ambayo alijitokeza mtu asiyetaka kuhesabiwa na kutatuliwa” alisema Mkuu huyo.

Hata hivyo mkuu huyo wa wilaya amesisitiza wananchi kuendelea kutoa ushrikiano kwa makarani hao wa sensa ili kufanikisha zoezi hilo la sensa ya watu na makazi litakalodumu kwa muda wa siku saba huku wilaya hiyo ikiwa na jumla ya kata thelathini.

Mwisho

BAADA YA KUSHINDA KESI IGUNGA CHADEMA YAWAPIGA MKWARA CCM




CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilitikisa Jimbo la Igunga mkoani Tabora, kwa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara ikiwa ni mara ya kwanza tangu Mahakama Kuu Kanda Tabora kutengua ubunge wa Dk Dalaly Kafumu wa Chama Cha Mapinduzi, huku kikiionya CCM kuwa kitaumbuka iwapo kitakata rufaa kwa uamuzi huo wa mahakama.

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika katika Viwanja vya Sokoine, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa alisema CCM kisithubutu kukata rufaa kwani kitaumbuka kwa kuwa kilicheza faulo nyingi katika uchaguzi huo.

Alisema ameshangazwa na kauli ya CCM kusema kuwa kitakata rufaa katika kesi hiyo wakati kisheria, kwa kesi za uchaguzi na pia katika hatua hiyo chama hakina nafasi yoyote bali mgombea au mwanachama wa chama husika, ndiye anayeweza kwenda mahakamani kufungua kesi na kupinga.

Katika mkutano huo uliofurika maelfu ya wanachama na washabiki wa wa chama hicho, Dk Slaa alisema kuwa Chadema kitakiangusha vibaya CCM hata ikiwa uchaguzi katika Jimbo la Igunga utarudiwa.

Huku akitoa mifano mbalimbali ya jinsi baadhi ya wanachama wa CCM walivyokuwa wakitoa rushwa, Dk Slaa alimtuhumu Mweka Hazina wa chama hicho, Mwigulu Nchemba, ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi kwamba alikuwa kinara wa kutoa rushwa katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Igunga Oktoba mwaka uliopita.

“Chadema imejipanga kwa rufaa hiyo ya CCM ikiwa ni pamoja na kufungua kesi nyingine dhidi ya vigogo wa CCM, walioshiriki katika kampeni za uchaguzi huo,”alisema Dk Slaa.

Dk Slaa pia alimponda Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama akieleza kuwa mdomo wake umemponza kwa sababu alikuwa akizungumza mambo ambayo hakujua madhara yake.

Wakati akitoa hukumu ya kesi hiyo, Jaji Mary Nsimbo Shangali wa Mahakama Kuu alisema moja ya hoja saba zilizotolewa na Chadema ambayo mahakama iliikubali ni ile ya Mukama kudai Chadema kilipeleka makomandoo katika uchaguzi huo na kupanga kuuvuruga.

Dk Slaa alisema: “Mukama alikurupuka kwa kutamka maneno bila kufanya utafiti hali iliyosababisha CCM kupoteza jimbo.”

Alikwenda mbali zaidi na kueleza kuwa suala la CCM kuingiza silaha ndani ya nchi, bila kibali wala leseni na kuwapatia vijana wake mafunzo katika kambi za Ilemo, Iramba mkoani Singida linamhusu mwenyekiti wa chama hicho na siyo mtu mwingine.

Alidai kuwa wakati wa uchaguzi wa Igunga, vijana hao walikuwa wakipewa mafunzo ya kijeshi akisisitiza kuwa suala hilo linamhusu mwenyekiti wa chama hicho akimtaka atoe majibu na ufafanuzi juu ya hilo.

Dk Slaa alisema kuwa siku ya jana ilikuwa ni kwa ajili ya wananchi wa Igunga kusherehekea na kupongezana kwa mshikamano waliouonyesha wakati wote wa kusikilizwa kwa kesi hiyo, huku akitoa pongezi kwa mawakili waliosimamia kesi hiyo kwa kuiwakilisha vyema Chadema katika kesi hiyo.

Naye upande wake aliyekuwa mgombea wa Chadema katika uchaguzi mdogo wa Igunga Oktoba mwaka uliopita, Joseph Kashindye aliwashukuru wananchi walioiunga mkono Chadema akieleza kuwa wameonyesha ushirikiano mkubwa uliokipa ushindi chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Kashindye aliwashukuru pia wananchi wa Igunga kwa kukichangia Chadema Sh6 milioni zilizosaidia kulipia gharama za kesi hiyo pamoja na malazi kwa mashahidi mbalimbali waliotoa ushahidi kwenye kesi dhidi ya CCM iliyotolewa hukumu wiki iliyopita kwa kutengua ushindi wa Dk Dalaly Kafumu wa CCM.

“Mahakama imetenda haki kwa kuwa imetoa hukumu ya haki…, nimeamini kuwa haki ya mtu haipotei. Awali nilidhani kuwa mahakama ni mali ya CCM kumbe si kweli,” alisema Kashindye na kushangiliwa na mamia ya watu waliofurika katika uwanja huo.

Kashindye aliponda ahadi zilizokuwa zikitolewa na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kwamba ndizo zilizofanya CCM kushindwa kesi.

“Watu wa ajabu sana, wametoa ahadi za kujenga madaraja, kusaidia chakula wakati hilo ni jukumu la Serikali,” alisema Kashindye akionyesha kushangaa.

Alibainisha kuwa wakati kesi hiyo ikinguruma mahakamani, alikuwa akitafutwa na wanachama wa CCM, lakini kutokana na kujua mbinu zao, aliamua kujichimbia kusikojulikana.

Dk Kafumu aliibuka mshindi katika uchaguzi huo mdogo uliofanyika Oktoba 2, mwaka jana kuziba nafasi ya Rostam Aziz ambaye alijiuzulu kwa madai kwamba anaachana na siasa chafu ndani ya CCM.

Katika uchaguzi huo kulikuwa na upinzani mkubwa kati ya Dk Kafumu na aliyekuwa mgombea wa Chadema, Joseph Kashindye ambaye hakuridhishwa na mwenendo wa uchaguzi huo, hivyo kuamua kupinga matokeo hayo mahakamani. Kesi hiyo ilifunguliwa Machi 26, mwaka huu.

 

Sunday, August 26, 2012

LEO NI SIKU YA SENSA KITAIFA


Karani wa Sensa akijaza takwimu muhimu za sensa katika Dodoso, hapo ni nyumbani kwa mkurugenzi wa Standard Radio Fm Bw. Prosper Kwigize mjini Kasulu mkoani Kigoma

Standard Radio fm

The Voice of Voiceless

90.1 mhz

SINGIDA TANZANIA

 

UONGOZI WA MAKAMPUNI YA BUHANZO ENTERPRISES, STANDARD VOICE LTD NA STANDARD RADIO FM TUNAWATAKIA WATANZANIA USHIRIKI MZURI WA ZOEZI LA SENSA YA WATU NA MAKAZI KWA AJILI YA KUPATA TAKWIMU SAHIHI KWA MAENDELEO

TUNAWASIHI WATANZANIA KUJIOKEZA KUSHIRIKI ZOEZI HILI

Friday, August 24, 2012

WAHADZABE KUGAWIWA KITOWEO ILI KUFANIKISHA SENSA



Na. Halma Jamal
Singida

SERIKALI ya wilaya mpya  Mkalama mkoani Singida, imeahidi kutoa nyama pori ya kutosha kwa Wahadzabe wa kitongoji cha Kipamba kata ya Mwangeza, ili waweze kushiriki sensa ya kitaifa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika nchini kote agosti 26 mwaka huu.

Mkuu wa wilaya hiyo Edward Ole Lenga,amesema msaada wa nyama ya wanyama pori hiyo, utasaidia jamii ya Wahdzabe kubaki kwenye kaya zao kipindi chote cha sensa.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kumkaribisha mkuu wa mkoa wa SIngida, Dk. Parseko Kone, awahamasishe  Wadzabe na wakazi wengine wa kata ya Munguli, kushiriki sensa,Lenga alisema msaada huo wa  nyama pori, unatokana na ombi liliotolewa na jamii hiyo ambayo chakula chake kikuu ni,nyamapori,mizizi,matunda pori na asali.

Akifafanua, alisema Wahdzabe hao wanaokadiriwa kufikia 227, wametoa ombi hilo ili wakati wote wa sensa wasiende porini kuwinda na badala yake wabaki kwenye kaya zao wakisubiri kuhesabiwa.

“Mheshimiwa mkuu wa mkoa, ndugu zetu hawa Wahdzabe, waliomba wapatiwe nyamapori ambayo ndiyo chakula chao kikuu, ili siku ya sensa wasiende kuwinda porini, kwa kweli endapo watapatiwa nyama hiyo, wamenihakikishia watabaki majumbani kusubiri makarani wa sensa”,alisema.

Mkuu huyo wa wilaya,alisema ombi hilo tayari limeishakubaliwa na maandalizi yote muhimu ya kuwinda wanyama pori siku moja kabla ya siku ya sensa, yamekwisha kamilika.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa Dk. Kone, yeyey alitoa msaada wa chakula chenye uzito wa zaidi ya tani moja, ambacho kitakidhi mahitaji kuanzia sasa hadi zoezi la sensa litakapokamilika.

“nimewaletea hiki chakula amacho ni mchele uliochangwa na vyakula mbali mbali ikiwemo pia mboga mboga ,kutoka shirika lisilo la kiserikali la International  Africa Outreach la nchini  Marekani. Chakula hiki  ni kizuri mno, kina virutubisho vingi”alifafanua Dk.Kone. 

Alisema kwa hali hiyo, kipindi chote cha sensa, hapatakuwepo na haja kwenda porini kutafuta wanyama pori, asali, matunda pori au mizizi.

Katika hatua nyingine,aliwataka wahakikishe kila mmoja anahesabiwa mara moja tu, kwa madai kuwa wakishafahamika idadi yao na hali zao za  maisha, itasaidia serikali kujipanga namna bora  ya kuwahudumia na kuwaletea maendeleo.

Wakati huo huo Dk. Kone, alisema pamoja na kunid la wawindaji, pia makundi mengine ya wavuvi, wachungaji wanaohama hama hama, watafutaji madini na baadhi ya wakulima ambao wana mashamba yaliyo mbali na makazi au makambi yoa ya kawaida, warejee kwenye kaya na makambi yao,ili waweze kuhesabiwa siku ya sensa.

BROTHERS OF CHARITY - SAINT DYPHMNA PSYCIATRIC CENTRE(MARUMBA/TANZANIA)


 
BROTHERS OF CHARITY

 

SAINT DYPHMNA PSYCIATRIC HEALTH CENTRE

 

(MARUMBA-TANZANIA)


        Construction of a Psychiatric sanitary structure which is adapted at the social condition of the milieu.

        To give some ambulatory care and to admit some acute and chronic patient as well as people with epilepsy.

        Formation of qualified workers.

         Sensibilization of  local population for their participation in care for their children with mental disorder.

        To promote a psychiatric sector with a religious vision, dynamic and ready to make a closer collaboration with other health institution.

        To develop an income generating through micro-projects for  local population.

        Sensibilization of local communities in the field of mental health.

        Visit and support to patient with mental disorder in their families.

 

PRESENT ACTIVITIES AND PROGRAMMES

          Welcome: Interviews

          Consultation out patient: Diagnosis, therapeutic project

          Admission in patient: To give shelter,Medications,food,clothes, nursing care

          Laboratory: Complementary examination, EEG,blood slide

          Pharmacy: Distribution of medicine for: In patient out patient Indigents

          Group therapy:Sensibilization,mental disorder,epilepsy,acceptance,counselling and guidance

          ergo therapy: Farming,agriculture,fishpound,cleaningKnitting

          Pastoral care:Masses,Choir,spiritual guidance, mutual support

          Formation: Training for the co-workers, training for local population, student's training

          Therapeutic community: Housing, clothing, medication, food Activities

TARGET GROUP

          Our target group is vulnerable people:

          Psychiatric patient (acute and chronic)

          People with epilepsy

          Local population

DIFFERENTIAL DIAGNOSIS OF:  NEW CASES, OLD CASES AND AMBULATORIES NEW CASES.

          EPILEPSY

          ACUTE PSYCHOSIS

          SCHIZOPHRENIA

          TOXICOMANY

          MENTAL RETARDATION

          DEMENCE SENILLE

          DEPRESSION

          BIPOLAR

          ANXIETY

          ALCOHOLISM

          There are different pathologies in SDPC. The first one is: ‘’Epilepsy’’. SDPC is known as a subject which stabilize people who are suffering from Epilepsy, Psychosis and Schizophrenia. The centre receives also the Toxicomanies because Toxicomany has been observed in Kigoma region and its really affect peoples more especially young ones.

 

 

Thursday, August 23, 2012

MASHIRIKA YA KIJAMII -SINGIDA



Na. Halima Jamal
Singida
SERIKALI wilayani Singida, imeahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGos) ikiwemo shirika la World vision, ili kuharakisha upatikanaji wa maendeleo endelevu kwa wakazi wa wilaya hiyo.
Ahadi hiyo imetolewa juzi na mkuu wa wilaya ya singida, Queen Mlozi, wakati akifungua warsha ya siku tatu iliyohusu kuwasilisha mpango wa STF/EMLAP unaotekelezwa na shirika la World vision.
Alisema mlango wa ofisi yake upo wazi wakati wote kwa mashirika yasiyo ya kiserikali na wadau mbali mbali wa maendeleo, katika kushirikiana kutatua kero zinazowakabili wananchi.
“Mimi naomba tufanye kazi kama timu moja, wimbo wetu uwe moja, nao ni kuwaletea wananchi wetu maendeleo ya kweli.  Kwa njia hii, tutaharakisha kuboresha maisha ya  wananchi  kiuchumi na kijamii",lifafanua Mlozi.
  Dc huyo alifafanua zaidi kwa kusema, serikali kwa upande wake, haina uwezo wa kutosha kufanya kila kitu kwa maendeleo ya wananchi, kwa hiyo ushirikiano wa NGos na wadau wengine, ni muhimu mno.
Katika hatua nyingine, Mlozi alitumia fursa hiyo kulipongeza shirika la World vision kwa juhudi zake za makusudi  kuanzisha miradi mbali mbali wilayani Singida na hasa katika tarafa ya Mtinko.
“Wananchi wa wilaya ya Singida, tunapaswa kutunza na kuilinda miradi hii iliyoanzishwa na World vision, iweze kudumu kwa muda mrefu.  Kwa njia hii, tutakuwa tunawatia moyo wenzetu wa World vision kuendelea kuleta neema ya miradi zaidi wilayani kwetu”,alisema.
Awali mratibu wa World vision Mtinko ADP,Edwin Maleko, alisema kwa mwaka huu, wametumia zaidi ya shilingi milioni 107.8 kugharamia utekelezaji wa mradi wa afya katika tarafa ya Mtinko.
Alitaja baadhi ya shughuli walizotekeleza kuwa ni kutoa mafunzo kwa vitendo kwa vikundi 51 vya lishe kuhusu njia sahihi za ulishaji wa watoto wadogo na wachanga na kugharamia kilniki tembezi 22 kwa vijiji vya Minyenye na Mughanga.
Maleko alitaja shughuli zingine kuwa ni kukarabati mtando wa maji unaohudumia vijiji vya Mtinko,Nduu,Malolo na Kijota na kuwezesha michezo ya mpira wa miguu,pete na kikapu baina ya vijana wa vijiji 19 ,kwa lengo la kutoa ujumbe unaohusu VVU na UKIMWI.
MWISHO.

WAPINZANI WAMTETEA LOWASA


MWENYEKITI wa Chama cha United Peoples Democratic (UPDP), Fahmi Dovutwa, amemfananisha Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na Waziri Mkuu Mstaafu, marehemu Rashid Kawawa.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Dovutwa alisema Lowassa hana tofauti na Kawawa, ambaye katika uhai wake akiwa waziri mkuu alibeba lawama za Serikali katika utawala wa awamu ya kwanza.

Dovutwa ambaye mwaka 2010 aligombea urais, alisema Lowassa hakuhusika katika kashfa ya rushwa iliyotokana na mkataba tata wa Richmond na kwamba alijiuzulu uwaziri mkuu ili kulinda heshima ya Serikali na si vinginevyo.

“Mwalimu Nyerere alipata kutoa hotuba siku moja akisema kwamba: ‘Namshukuru sana mzee Rashidi Mfaume Kawawa, amenisaidia sana.
‘Mambo yote ambayo amekuwa akilaumiwa Kawawa niliyafanya mimi na yeye (Kawawa) alibeba tuhuma hizo kwa ajili yangu’, haya ni maneno ya Baba wa Taifa na hotuba zake hizi zipo,” alisema Dovutwa akimnukuu Mwalimu.

Dovutwa aliongeza: “Kwa kauli hiyo ya Baba wa Taifa ni wazi Lowassa hakuhusika na kashfa ya Richmond. Kwa sababu maamuzi ya kiutendaji wa Serikali yako mikononi mwa Baraza la Mawaziri ambalo mwenyekiti wake ni Rais.

“Waziri yeyote hana uwezo wala mamlaka ya kuamua jambo bila ridhaa ya Rais. Lowassa aliwajibika ili kuilinda Serikali ya CCM chini ya Rais Kikwete isianguke na kupisha uchaguzi mwingine,” alisema.

“Mwalimu Nyerere alielewa vizuri dhana ya uwajibikaji na Watanzania wengi hawakumwelewa Mwalimu Nyerere alipokuwa akiwarudisha baadhi ya watumishi ambao awali waliwajibika kwa tuhuma za kiutumishi.

“Kimsingi tuhuma alizokuwa amelaumiwa kiongozi mwandamizi wa Serikali zilikuwa ni tuhuma za kiongozi mkuu wa Serikali ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kuamua kufanya jambo au kulikataa.

“Ili kuilinda Serikali na kiongozi mkuu wa Serikali ndipo hutokea mtumishi mmoja wa Serikali kubeba lawama na tuhuma za wizara yake kwa manufaa ya Serikali yenyewe.

Hivyo dhana ya kuwajibika ilieleweka vizuri kwa Mwalimu Nyerere kuliko wasomi walio wengi wa ndani na nje ya CCM,” alisema Dovutwa.

Dovutwa alisema Lowassa ni kiongozi makini mwenye ujasiri ambaye aliweza kufanya mambo akiwa waziri mkuu, huku akiwatahadharisha wananchi kuwa makini na baadhi ya viongozi.

“Watanzania tusikumbuke kufanya mabadiliko ambayo huenda tukaondoa wala rushwa wadogo na kuingiza wala rushwa wakubwa zaidi,” alisema.

Dovutwa aliwataka Watanzania kutafakari juu ya mwenendo wa vyama vilivyoko bungeni, hasa kutokana na Bunge kuchafuka kutokana na kashfa ya rushwa inayowahusisha wabunge.

Wednesday, August 22, 2012

What Burundi could teach Rwanda about reconciliation

Peter Nkurunziza
President of Republic of Burundi

As african country we should have enough time to think on our problem and how to recover lather than still fighting, one mistake made by one of the african country should be a lesson to another, But what Burundi could teach Rwanda? please follow this story from Bujumbura

 

Rose Hakizimana's photo album documenting the massacre of Tutsis in Burundi in 1993

Related Stories


Rose Hakizimana's mother and four sisters were killed by Burundian Hutu rebels while they were housed in a camp for ethnic Tutsis forced to flee their homes.

She remembers finding her mother's body by identifying her legs. For a full year after the burial she had nightmares.

When people think of genocide in Africa, neighbouring Rwanda usually comes to mind after the slaughter of some 800,000 Tutsi and moderate Hutus in 100 days in 1994.

Start Quote

Rose Hakizimana
What we are seeing now is a government that is not against Hutu or Tutsi, but a government that targets individuals who don't agree with their policies”
End Quote Rose Hakizimana Burundian political commentator

But over the years Burundi, which has a similar ethnic make-up and tensions, has also faced killings by both Tutsi and Hutus, driving a wedge into the fabric of the nation.

The most shocking was in 1972, when some estimate up to 300,000 Hutus were massacred in six weeks.

Ms Hazikimana has kept an album documenting acts of genocide in 1993 in which some 25,000 Tutsis are believed to have died, so that the crimes are not forgotten.

She went on to become an MP in the transitional government that brought peace to Burundi.

Now retired, she has a regular slot on local radio as a political commentator and says ethnicity is no longer an issue in politics.

"If you look at the current situation in the country, though we have a Hutu-dominated government that is not the problem," she told the BBC.

"What we are seeing now is a government that is not against Hutu or Tutsi, but a government that targets individuals who don't agree with their policies."

Her comments reveal how Burundi is now coping with ethnicity far better than its better-known neighbour.

Fifty years of killing

Map
Burundi:
  • 1965: More than 80 leading Hutu politicians shot after an abortive coup
  • 1972: Between 150,000 and 300,000 mainly Hutus killed following an insurgency
  • 1988: Between 15,000 and 25,000 mainly Hutus killed after violence in the north
  • 1993: Some 25,000 Tutsis killed following the assassination of Hutu President Melchoir Ndadaye by Tutsi soldiers
Rwanda:
  • 1959: Thousands of Tutsis killed following a Hutu revolt
  • 1963: Between 10,000 and 20,000 Tutsis killed after an incursion by pro-monarchist Tutsi rebels based in Burundi
  • 1991: Hundreds of Bagogwe - a Tutsi subgroup - killed over several months in the north-west following an invasion by Tutsi rebels based in Uganda
  • 1994: 800,000 mainly Tutsis and moderate Hutus killed in 100 days
  • 1995: Rwanda's new armed forces attack Kibeho camp housing Hutu refugees - some 5,000 people killed and more than 20,000 others died after fleeing the camp
  • 1996: Rwanda troops invade Zaire, now DR Congo, to pursue Hutu militia involved in the genocide. Thousands of Hutus killed
First Hutu army chief
This may be down to the Arusha Peace Accord, brokered by South Africa's former President Nelson Mandela.

Signed in August 2000, the ceasefire led to talks that eventually helped end the long, drawn-out conflict and got politicians from both sides of the ethnic divide talking - it put ethnicity centre stage.

The accord recognised the tensions between the dominant Tutsi minority and the Hutu majority as a catalyst to the conflict and came up with a 60-40 formula of proportional representation.

Two years ago, ex-rebel Godefroid Niyombare became the first ever Hutu army chief of general staff.

According to President Pierre Nkurunziza - a former rebel Hutu leader who came to power in the first democratic elections in 2005 - this new-look army is a testimony to reconciliation efforts.

"The base of our problems during former times were the army and the police - now we have both ethnic groups represented," the president told the BBC.

Such a comment from Rwanda's President Paul Kagame would be unthinkable, as tribal references are banned and considered tantamount to a denial of the genocide - a criminal offence.

A Rwandan opposition leader is currently on trial for propagating ethnic hatred because she has questioned why the official memorial to the 1994 genocide only mentions the Tutsis killed, not the Hutu victims.

Mr Kagame says such strong-arm tactics are needed to prevent a repeat of the massacres, but his critics say he is only keeping a lid on the tensions, which could boil over.
Ethnic jokes
In Burundi where it was once also a taboo to mention ethnicity, politicians now make light of their ethnic differences in public debates, something analysts say has contributed to the healing process.

Rebuilding and reshaping Rwanda

For example, traditionally Tutsis, who reared cattle, were thought to drink more milk than Hutus, who were farmers.

So a Tutsi might jest with a Hutu colleague who reaches out for the milk during an office tea-break: "You Hutus, you want to drink all the milk now."

Such banter, even in a bar, would be careless talk in Rwanda that could land you in jail.

This is not to say that Rwanda is not witnessing some reconciliation.

The show village of Bugesera, outside the Rwandan capital of Kigali, is an example.

Set up by a non-governmental organisation to show that enemies can live as neighbours, it has been Laurence Niyongira's home for the last 10 years.

The killers of her family are not only her friends, but people she now refers to as family.

Her neighbour's husband organised the killing of her family - a fact both families cannot hide.

"[But] we have reached reconciliation and have forgiven each other," she admits - words often repeated from other Bugesera residents.
Truth and reconciliation
Rwanda has also made much more progress when it comes to seeking justice for genocide victims, setting up community "gacaca" courts which tried close to two million people for their involvement.

Photos of victims of the Rwandan 1994 genocide Unlike Rwanda, Burundi does not have that many visible massacre memorials

In contrast Burundi has been slow in setting up national institutions to deal with the crimes committed.

But the government hopes that once there is funding and systems in place they will be able to let justice take its course - a Truth and Reconciliation Commission has been promised.

And unlike its neighbour, the symbols of reconciliation are not many or that obvious.

There is a mausoleum in the capital, Bujumbura, to remember Melchior Ndadaye - the first democratically elected Hutu president, who was assassinated in October 1993 by Tutsi soldiers.

Mausoleum for Melchior Ndadaye Melchior Ndadaye was Burundi's first democratically elected Hutu president - assassinated in 1993

A similar monument honours independence hero Louis Rwagsore, a royal prince who won respect from both the Tutsi and Hutu communities.

But the ethnic divide that Burundi experienced - with Tutsis dominating every sphere of society and neighbourhoods split along ethnic lines - is all but over.

Burundians consider themselves to be free and are confident that their country will not be torn apart by ethnic enmity again.

Human rights bodies like Amnesty International laud Burundi for embracing democracy and having a much better grasp of it than Rwanda.

For Ms Hazikimana, who knows that the former rebels now in power killed her family, the root cause of the misdeeds of Burundi's past was never ethnicity.

"Burundians never hated each other. It was all about politics and done for political gain. Politicians used money to convince people to carry out crimes and killings."

WAZIRI Mkuu wa Ethiopia, Meles Zenawi (57), amefariki dunia juzi usiku mjini Brussels, Ubelgiji alikokuwa akitibiwa.Taarifa iliyotangazwa na Televisheni ya Taifa ya Ethiopia, imeeleza kuwa Zenawi alifariki dunia saa 5:15 usiku.

Kutokana na Katiba ya nchi hiyo, nafasi ya kiongozi huyo mwenye historia ya kipekee nchini humo, itashikiliwa na Naibu Waziri Mkuu, Hailemariam Desalegn.

Mpaka anakutwa na mauti, hakuna taarifa zozote ambazo zilithibitisha hasa ugonjwa uliosababisha kifo chake. Kiongozi huyo alikuwa madarakani tangu mwaka 1991 alipompindua Mengistu Haile Mariam.
Hata hivyo, taarifa ambazo hazijathibitishwa zinaeleza kuwa Zenawi alikuwa akisumbuliwa na uvimbe kwenye ubongo.

Habari kwamba kiongozi huyo wa zamani wa vita ya msituni alikuwa mgonjwa, zilianza kusambaa tangu aliposhindwa kuhudhuria mkutano wa kilele wa Umoja wa Afrika, Addis Ababa mwezi uliopita.
Tangu kipindi hicho, wasiwasi ulitanda nchini humo hasa alipochukua likizo. Uvumi huo ulipingwa na Msemaji wa Serikali ya Ethiopia, Bereket Semon ambaye amekuwa akirejea kauli yake hiyo ya kupinga uvumi mara kwa mara.

Msemaji huyo amekuwa akisisitiza kuwa afya ya kiongozi huyo haikuwa mbaya kama ilivyokuwa ikidaiwa na kusisitiza kwamba alichukua likizo baada ya kupewa ushauri na daktari.
Zenawi atakumbukwa kwa sera yake ya kiutawala ambayo ilijulikana kama ‘shirikisho la makabila,’ iliyoyafanya makabila mbalimbali ya nchi hiyo kujitawala yenyewe, lakini bado utawala wake uliendelea kuwa na nguvu.

Zenawi alikuwa mwanasiasa mjanja ambaye aliipenda siasa tangu akiwa kijana mdogo. Alitokea kwenye kundi maarufu la TPLF, ambalo lilikuwa likiongoza mapambano dhidi ya utawala wa kijeshi wa Ethiopia miaka ya 1970 na 1980.

Kiongozi huyo aliyeacha watoto watatu, aliwahi kutajwa kama mmoja wa viongozi wenye ushawishi mkubwa na ambaye utawala wake ulikumbwa na utata barani Afrika.

Wakati Zenawi anafariki dunia, Naibu Waziri Mkuu, Desalegn alikuwa katika mkutano China.
Katika hatua nyingine, Serikali ya Ethiopia ilisema kwamba haitafanya uchaguzi kwa kuwa viongozi waliopo wako imara.

Simon alisema kwa sasa Serikali inashughulika na mazishi ya kiongozi huyo na kwamba mwisho wake wa kuwa madarakani kwa mujibu wa katiba ni mwaka 2015.

“Hakuna wasiwasi wowote na uongozi uliopo madarakani kwani chama kilichopo madarakani kipo katika hali nzuri na kina viongozi imara,” alisema.
Source: mwananchi

MAHAKAMA KUU YAISHIKA PABAYA CCM

Dr. Peter Kafumu
 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimepata pigo baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Tabora, kutengua matokeo ya ubunge Jimbo la Igunga yaliyompa ushindi mgombea wake, Dk Dalaly Peter Kafumu.Dk Kafumu aliibuka mshindi katika uchaguzi mdogo uliofanyika Oktoba 2, mwaka jana kuziba nafasi ya Rostam Aziz ambaye alijiuzulu kwa madai kwamba anaachana na siasa chafu ndani ya CCM.

Uchaguzi huo ulikuwa wa ushindani mkubwa kati ya Dk Kafumu na aliyekuwa mgombea wa Chadema, Joseph Kashindye ambaye hakuridhishwa na mwenendo wa uchaguzi huo, hivyo kuamua kupinga matokeo hayo mahakamani. Kesi hiyo ilifunguliwa Machi 26, mwaka huu.

Akitoa hukumu hiyo, Jaji Mary Nsimbo Shangali alisema Mahakama ilipokea malalamiko 15 ambayo yaliridhiwa na pande zote mbili, lakini baadaye yakaongezwa madai mengine mawili hivyo kufikia 17.
“Madai yaliyopokewa na Mahakama ni 17 na kati yake imethibitisha madai saba,” alisema Jaji Shangali katika hukumu hiyo.

Mbali na Dk Kafumu, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ya uchaguzi walikuwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Igunga aliyetangaza matokeo hayo.
Dk Kafumu akizungumza na Radio One jana alisema tangu awali, hakuwa na imani na jaji aliyesikiliza kesi hiyo. Alisema hana mpango wa kukata rufaa, bali anawaachia viongozi wa CCM kufanya hilo.
Alisema baada ya ubunge wake kutenguliwa, anaendelea na shughuli zake za madini kwa kuwa ni mtaalamu wa sekta hiyo... “Ndugu mwandishi karibu Singida, mimi narudi kuendelea na shughuli zangu za madini.”
Sababu za kutengua matokeo
Alisema hoja zilizothibitishwa na Mahakama na ambazo zimetumika kutengua matokeo hayo ni pamoja madai kwamba Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli alitumia nafasi yake ya uwaziri kutoa ahadi ya ujenzi wa Daraja la Mbutu ambalo lilikuwa ni moja ya kero kubwa kwa wananchi wa Jimbo la Igunga.

Dk Magufuli akiwa katika moja ya kampeni za uchaguzi huo, alitumia nafasi ya uwaziri kwa kuwatisha wapigakura wa jimbo hilo kwa kusema kama hawatamchagua mgombea wa CCM, watawekwa ndani.

Jaji Shangali aliendelea kueleza kuwa Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage alitangaza kuwa mgombea wa Chadema alikuwa amejitoa katika uchaguzi huo, jambo ambalo Mahakama imeridhishwa na ushahidi uliokuwa ukitolewa.

Jaji Shangali alitaja hoja nyingine iliyotumika kufuta matokeo hayo kuwa ni kauli ya Imamu Swaleh Mohamed wa Msikiti wa Ijumaa Igunga, kuwatangazia waumini wa msikiti huo kuwa wasikichague Chadema, kwa kuwa baadhi ya viongozi wake wamemdhalilisha Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Fatuma Kimario.Alisema hoja nyingine ni Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama kudai kuwa Chadema kilileta makomandoo katika uchaguzi huo na kupanga kuuvuruga.

Hoja nyingine ambayo Jaji Shangali aliikubali ni ugawaji wa mahindi ya kuwawezesha wakazi wa Igunga kukabiliana na njaa wakati wa uchaguzi huo kwamba ulitumiwa vibaya na baadhi ya wanasiasa kuwashawishi wananchi wawapigie kura.

Jaji huyo alihoji iwapo wakazi wa Jimbo la Igunga walikuwa na njaa sana wakati wa uchaguzi huo kiasi cha viongozi wa Serikali kuona kuwa ulikuwa wakati mwafaka wa kugawa mahindi hayo.
Kuhusu hoja ya upande wa utetezi kwamba mgombea wa Chadema, Kashindye alipaswa kupeleka malalamiko hayo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), alisema siyo ya msingi yanayoweza kumzuia mlalamikaji kupeleka malalamiko hayo katika Mahakama Kuu na hakuna kifungu chochote kinachomzuia mlalamikaji kufanya hivyo.

Kutokana na hali hiyo, Jaji Shangali alisema kuanzia sasa Jimbo la Igunga lipo wazi na kwamba: “Milango iko wazi kwa walalamikiwa kukata rufaa ikiwa hawajaridhika na uamuzi.”

Hali ya usalama katika mahakama hiyo ilikuwa imeimarishwa, huku wafuasi wa Chadema wakiwa wengi zaidi na wakionekana kuwa na furaha hasa baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo.

Dk Slaa, Nape wazungumza
Baada ya hukumu hiyo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alisema: “Mahakama imedhihirisha yale ambayo tumekuwa tukisema kila wakati kwamba CCM inatumia mabavu.”

Alisema anashukuru Mahakama kwa kutoa haki na kukubaliana na Chadema kuwa CCM iligawa vyakula kwa wananchi ili kuwashawishi wawapigie kura.

Pia alisema kwamba imeudhihirishia umma kauli kwamba CCM kinatumia vibaya rasilimali za nchi katika mambo ya siasa akitoa mfano wa mawaziri kuwalazimisha watu wawachague wagombea wao.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema alikuwa hana taarifa kuhusu hukumu ya kesi hiyo.
Hata alipopata taarifa kuhusu matokeo hayo, alisema atakuwa tayari kuyazungumzia pindi akiyapata kutoka katika mfumo wa chama chao.“Siwezi kuzungumzia matokeo ya hukumu unayoniambia wewe. Nitakuwa tayari pindi nitakapoyapata rasmi kutoka kule Igunga (CCM),” alisema Nape.

Uchaguzi
Oktoba 3 mwaka jana Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Igunga, Magayane Protas alimtangaza Dk Kafumu kushinda ubunge kwa kura 26,484 akifuatiwa na Kashindye ambaye alipata kura 23,260, huku Leopold Mahona wa CUF akipata kura 2,104.

Ushindi huo wa CCM ulihitimisha mojawapo ya michuano mikali ya kisiasa nchini ambayo Chadema, CUF na CCM vilionekana kufukuzana vikali. Dk Kafumu kabla ya nafasi yake hiyo alikuwa Kamishna wa Madini katika Wizara ya Nishati na Madini.

Ushindi wa CCM katika jimbo hilo ulikuwa ni pigo kubwa kwa Chadema kwani ulikifanya chama hicho kushindwa kuibuka na ushindi hata katika mazingira ambayo kilitarajiwa au kuonekana kukubalika zaidi. Chaguzi nyingine ambazo Chadema kilidhaniwa kushinda ni zile za Babati, Busanda na Biharamulo ambako kote CCM kilitetea viti vyake.
Nyongeza na Leon Bahati.
 
source: mwananchi

Tuesday, August 21, 2012

VILOBA VINATAFUNA NGUVU KAZI YA TAIFA


“Nimeteseka sana, nimetengwa sana, na nimeumizwa sana pamoja na kuwaumiza wenzangu, yote haya ni kwa sababu ya matumizi ya madawa ya kulevya, pombe kali hasa viloba hadi akili yangu ikaharibika nikajikuta nimekuwa mwehu nikitembea hovyo mitaani, kutukana na hata kupigana, hakika kwa sasa ninalo funzo kwa vijana wenzangu”

Hii ni Kauli ya kijana mmoja kutoka Dar es salaam ambaye sasa anatibiwa na kutunzwa katika kijiji cha Marumba wilayani Kasulu ambako alifikishwa na ndugu zake miezi kadhaa iliyopita baada ya kuugua ugonjwa wa akili na sasa akili yake japo kwa mwendo wa kinyonga inaanza kurejea.

Matumizi ya pombe kali VILOBA ni moja ya chanzo cha vijana wengi kuwa na matatizo ya akili na hata kupoteza afya ya mwili pia, si ajabu kuwakuta wapenzi na wanywaji wa viloba wakiwa maumbile yaliyokonda na kuchoka, kuungua midomo na hata kunyonyoa nywele, kukosa uwezo wa kufikiri na mwili kukosa nguvu

Si ajabu kumkuta kijana mpiga viloba akitetemeka mwili kila wakati anaposhika au kubeba chochote mikononi mwake, wengu wanashindwa hata kufanya kazi yoyote

Taifa limepoteza nguvu kazi kutokana na viloba na ulevi mwingine wa kupindukia pamoja na matumizi ya madawa ya kulevya,

Hii ndiyo sababu shirika la kitawa la BROTHERS OF CHARITY liliamua kuanzisha kitengo cha afya ya akili na kuanza kutoa tiba ya magonjwa hayo pamoja na matunzo ya kijamii na kisaikolojia kwa wagonjwa wa akili maarufu kama WEHU.

PICHA