Sunday, January 27, 2013

BODA BODA WAPATA MAFUNZO YA UDEREVA


 
 
 
 
Mkuu wa chuo cha VETA Singida Afridon Mkhomoi, Akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo ya kutunuku vyeti wahitimu wa mafunzo ya udereva wilayani Mkalama.
Picha na Nathanael Limu
 
Serikali  wilayani Mkalama mkoani Singida, imekipongeza chuo cha mafunzo ya ufundi stadi (VETA) Singida, kwa uamuzi wake wa kuanza kuwafuata wateja mahali walipo, badala ya kuwasubiri waje chuoni.

Pongezi hizo zimetolewa na mkuu wilaya hiyo, Bw Edward Ole Lenga wakati akizungumza kwenye halfa ya kufunga mafunzo ya waendesha pikipiki (Bodaboda) iliyofanyika Nduguti, makao makuu ya wilaya mpya ya Mkalama.

Katika hotuba ya Bw. Lenga iliyosomwa kwa niaba yake na mkuu wa kituo cha polisi  Mkalama Bw. Michael Marwa, amesema uamuzi huo wa busara wa kumfuata mteja mahali alipo, una faida nyingi ikiwemo ya kutoathiri shughuli za mteja

Katika hatua nyingine, mkuu huyo wa wilaya, ametoa rai kwa wakazi wote wa wilaya ya Mkalama wanaomiliki na kuendesha pikipiki, magari au vyombo vya moto, kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika kila kata, ili waweze kuletewa mafunzo.
Awali mkuu wa chuo cha VETA Singida Afridon Mkhomoi, amesema mafunzo yanayotolewa na VETA yanalenga kukidhi sera ya nchi ya kuwawezesha vijana kujiajiri na kuwa wajasiriamali.  

1 comment:

Anonymous said...

I'm gone to say to my little brother, that he should also go to see this website on regular basis to obtain updated from hottest news.

freitag hoskins declared whitacre teamplayer
http://showcase.fr/standard-specifics-cheap-twitter-followers-free
http://tourserver.org/node/22164
http://www.40jesus.net/d/node/7848
http://damida.co.il/node/41665
http://networkbuffalo.com/v2/cheap-twitter-followers-free-or-wants
spain national team vacs sublimity resorces boogaloo

Feel free to surf to my blog post ... offical