Thursday, January 3, 2013

TUKIO LA MOTO MADUKANI SINGIDA KATIKA PICHA

 
 
Mkuu wa Mkoa Singida Dakta Paserko Kone ametangaza kuwa ataunda tume ya kufanya uchunguzi wa chanzo cha moto uliounguza nyumba ya shirika la nyumba la taifa na kusababisha hasara kubwa kwa wapangaji waliokuwa na maduka na makazi katika nyumba hiyo
 
 

 
 
Mkuu huyo wa mkoa amefikia azima hiyo baada ya kukosa habari sahihi za chanzo cha moto huo pamooja na kutaarifiwa kuwa kikosi cha zima moto mkoani Singida kimeshindwa kufika kwa wakati kuuzima moto huo kwa visingizio mbalimbali ikiwemo kukosa maji na uchakavu wa matari ya gari la kuzima moto
 
 
 
Mmoja wa wapangaji waliokuwa wanaishi na kufanya biashara ndani ya Nyumba hiyo ni pamoja na Bi Aida Mlei ambaye alifanikiwa kumwokoa mwanae mwenye umri wa miaka mitano amesema kuwa yeye hajui nini hasa chanzo cha moto huo kwani mwanae huyo ndiye alikuwa anaangalia runigna sebuleni ambako kulikuwa na makochi, jiko la umeme na gesi, kabati la vyombo, magunia ya mchele ambavyo vimeteketea vyote
 
 
Kwa mujibu wa jirani wa nyumba hiyo Bwana Saduni Halfani amesema kuwa zima moto zilizotumika zimetoka majumbani kwao kwani gari la zima moto lilishindwa kutoa huduma hiyo kwa kuwa na matatizo yaliyosemekana kuwa ni ya kiufundi
hili ni tukio la pili kwa nyumba ya biashara kuungua moto mjini singida katika eneo la soko kuu, na lawama zote kupelekwa kwa kikosi cha zima moto
 
Kwa upande wake Kamanda wa Kikosi cha kuzima moto Bwana Kelvin Mapunda amekiri kuwa gari la zima moto lilikuwa na matatizo ya matairi hatimaye kushindwa kutoa msaada wakati wa ajali hiyo
huyu ni mmoja wa wananchi ambaye alijitosa ndani ya nyumba hiyo kujaribu kuokoa uhai wa binadamu, hata hivyo alipata majeraha na kupata huduma ya kwanza.
 
Taarifa za awali zinaonesha kuwa, hakuna kifo kilichotokea na thamaniya mali zilizoharibiwa haijafahamika.
 
Standard Radio Itaendelea kufuatilia na kuendelea kukuletea taarifa zaidi
 
Habari hii imeandaliwa na EUFRASIA MATHIAS, SAADA SALUM MASOUD na SAMUEL LUCAS, Picha na Standard Radio FM

No comments: