Wednesday, January 9, 2013

KIKWETE AWAHIMIZA WANANCHI SINGIDA KULIMA KWA BIDII


 
Na Edilitruda Chami

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete  amewataka wananchi wa mkoa wa Singida kushiriki kikamilifu katika shughuli za kilimo, ili kuondokana na umaskini.

 

Wito huo ameutoa jana katika ibada ya kumuweka wakfu askofu wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania  KKKT mkoani singida,  Dr.Alex Nkumbo  iliyofanyika katika kanisa la msalaba mrefu {EMMANUELI} manispaa ya singida

 

Ameongeza kuwa  kwa kufanya hivyo umaskini utatoweka  na kwamba ni vyema wakatambua kuwa kilimo hakichagui mtu, kabila wala dini ila ni juhudi za mtu binafsi hivyo washikamane ili kuleta maendeleo kupitia kilimo

 

Ametaja mazao ambayo hustawi vizuri mkoani Singida kuwa ni alizeti, vitunguu, na pamba ambapo wengi wamekuwa hawajishughulishi na kilimo hicho.  

 

Wakati huo huo, askofu mpya wa KKKT usharika wa Emanuel dayosisi ya Kati Singida, Dr.Alex Nkumbo amekiri kufuata sheria za kanisa hilo mbele ya waumini  na viongozi  wa kanisa hilo nchini.

 

Amesema kuwa  atakuwa mvumilivu, jasiri, na mwenye moyo wa kujitolea  kwa mujibu na taratibu za nchi pamoja na kanisa hilo atatekeleza majukumu yote yaliyo ndani ya uwezo wake ikiwemo kuhimiza waumini kaushiriki katika shughuli za kilimo ipasavyo ili kunyanyua uchumi nchini Tanzania

 

Aidha maaskofu pamoja na wachungaji wa kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania  wamempokea kwa furaha na amani na kumhakikishia kuwa watampa ushirikiano kiongozi  huyo katika njanja mbalimbali za kimaendeleo mkoani singida na kuwa atakayekiuka na kuwa tofauti na dini yao atakuwa kinyume na matakwa yao kwani moja ya lengo la kanisa lao ni kuhimiza kilimo na kuhakikisha kila muumini anajishughulisha na kilimo

 

Waumini waliohudhuria katika ibada hiyo wamewashukuru viongozi wa serikali waliohudhuria katika ibada hiyo, bila kujali dini zao kama vile mkuu wa mkoa wa singida Dr Paseko Kone, Mh. Mohamed Dewji ambaye ni mbunge wa Singida,. wakuu wa wilaya, wabunge na watumishi wa serikali mkoani humo.                                                                                                              

No comments: