Monday, January 21, 2013

MKUU WA MKOA WA SINGIDA ACHACHAMAA


Mkuu wa mkoa wa Singida Dr, Parseko Kone ameonya tabia ya baadhi ya maafisa wa serikali na vyombo vya habari kutoa taarifa zisizo sahihi kwa wananchi
 
Dr. Kone amesema hayo jana katika hafla fupi ya kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013, iliyofanyika katika chuo cha utumishi wa Umma mjini Singida
 
Dr. Kone amesema hayo kufuatia vyombo vya habari kuripoti habari ya uhaba wa chakula mkoani Singida, na kutaja kuwa takwimu zilizotolewa katika habari iliyochapishwa na moja ya magazeti ya kil asiku si sahihi
 
Mwishoni mwa wiki, baraza la madiwani wilaya ya Singida lilikiri kuwepo kwa uhaba mkubwa wa chakula na kuagiza uongozi wa halmashauri hiyo kulitafutaia ufumbuzi mara moja
 

1 comment:

Prosper Ngairo said...

Mheshimiwa, sasa huyo mkuu wa mkoa mbona haeleweki?Baraza la madiwani limesema kuna njaa,yeye anakanusha tushike lipi?