Friday, January 25, 2013

WANAJESHI WA RWANDA WATEKWA KAGERA


Wanajeshi wa jeshi la Rwanda waliokuwa wakisafiri kutoka Kigari kwenda Dar es Salaam wamenusurika kifo baada ya watu wanaotajwa kuwa majambazi kuliteka gari walimokuwa wakisafiria


Tukio hilo limetokea alfajiri leo majira ya saa 12:45 asubuhi katika kijiji cha KIkoma Kata ya Lusahunga wilayani biharamulo moani Kagera


Katika tukio hilo jumla ya magari matano yametekwa na watu wenye silaha nzito za kivita


Akizungumuza Standard Radio kwa njia ya simu Diwani wa kata ya Lusahunga Bw. Amoni Mizengo amesema, wanajeshi hao wa Rwanda walikuwa wakisafiri kwenda Dar es salaam kununua magari.


Aidha askari mmoja wa jeshi la polisi Tanzania Kituo Cha Nyakahura wilayani Biharamlo ni miongoni mwa waliotekwa na kuporwa vitu mbalimbali


Mkuu wa jeshi la polisi mkoa wa Kagera ACP Phillip Kallang amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi                                        ENDS

No comments: