Friday, January 25, 2013

WAPANGAJI WA NYUMBA MKOANI SINGIDA WALALAMA


Baadhi ya wapangaji katika manispaa ya  singida wamelalamikia wenye nyumba kwa kuwanyanyasa na kuwadharau kwani na wao wanahitaji kuheshimiwa.ili waweze kuishi kwa huru kama watu wengine.

 

Hayo yamesemwa na mmoja wa wapangaji Bi.Rehema mussa alipozungumza na standard radio ambapo amesema kuwa wenye nyumba wamekuwa wakiwadharau wapangaji kwa kuwatolea kauli chafu, kitendo kinachowafanya  waishi bila amani na kuwa na hofu wakati wote.

 

Naye Bw. Haruna Issa amesema kuwa wenye nyumba ni lazima watambue kuwa wapangaji wanahitaji kuthaminiwa kwani wengi wao walikotoka wana nyumba pengine nzuri kuliko hata hizo.

 

Hata hivyo ameongeza kwa kusema kuwa wenye nyumba lazima wawe na msimamo katika  mapatano ili kuepusha usumbufu unaojitokeza kutokana na baadhi yao kubadilisha kodi kinyume na maelewano baina yao na wapangaji.

 

No comments: