Wednesday, January 16, 2013

MMOJA AFA KWA AJALI IRAMBA

Na. Halma Jamali
Singida

Mtu mmoja mkazi wa Kiomboi mkoani Singida Mkapa Jumanne 18,amefariki dunia papo hapo baada ya kurukia gari lililokuwa kwenye mwendo kasi.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani hapa Linus Sinzumwa amelitaja gari hilo kuwa ni Mini Bus Fuso lenye namba za usajili T.590 ABA lililokuwa linatoka maeneo ya Kinampanda madukani kuelekea Haydom katika wilaya mpya ya mkalama.

Alisema kuwa marehemu huyo ambaye ni konda wa gari hilo juzi tar 14,majira ya saa 9 alasiri alikuwa katika harakati za kupanda gari hilo wakati lipo kwenye mwendo na bahati mbaya alitereza na kuangukia katika tairi la nyuma la gari hilo na kupitiwa na kufariki papo hapo.

Aidha Sinzumwa alisema kuwa dereva wa gari hilo aliyejulikana kwa jina la Hereio Neema 42,anashikiliwa na jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi.

Kamanda huyo ametoa wito kwa madereva wanaoendesha vyombo vya moto kuwa makini ili kuepusha vifo vya watu wasio na hatia.

No comments: