Wednesday, January 2, 2013

SALAAM ZA MWAKA MPYA TOKA STANDARD RADIO

Wakati wa sikukuu ya Noeli na mwaka mpya mambo mengi hufanyanyika, kubwa zaidi huwa ni salaam kwa maradfiki, ndugu na hata kupeana zawadi

watumishi wa standard radio fm Singida wanatumia fursa hii kutoa ujumbe mhimu wa kutakiana heri ya Mwaka mpya.

FUATILIA SALAAM HIZI PAMOJA NA U JUMBE KUTOKA KWA WANA STANDARD

BONIFACE MPAGAPE: Uzuri na utamu wa ngoma, ingia lingoni ucheze! Shiriki kwa dhati katika kila suala linalohusu maendeleo ya jamii yako. Ninaomba ushirikiano wako ili tuweze kuleta mabadiliko katika jamii. Kheri ya Mwaka mpya 2013
 
 
 
 
 
Eufrasia mathias:Ugumu wa maisha ni kipimo cha akili, fanya kazi uonje matunda ya akili yako.
It is better to  be terminated because of hardworking than to be terminated because of laziness
 
 
 
 
Edilitruda Chami: Matokeo mazuri yankusubiri wewe ,tembea na malengo,kimbia kwa kujiamini mwaka 2013,paa ukitambua kuzaliwa maskini siyo kosa lako bali ukifa maskini ni kosa lako
 
 
 
 
Moses Anthony John: Namshukuru Mungu kwa kumaliza na kuanza mwaka vizuri , kuna mengi tumekumbana nayo na bado kuna mengi tutakutana nayo, mazuri kwa mabaya ila kwa uwezo wa Mungu tutasonga,Niwatakie kheri ya mwaka mpya STAFF wote wa SR na Buhanzo enterprises na watanzania wote
 
 
 
 
Zaituni M. Kimu: Bila Mwenyezi Mungu hakuna linalowezekana,  Namshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufikia Mwaka huu 2013, Na wale ambao Mwenyezi Mungu hakupenda wafikie mwaka huu 2013 tuwaombee wawe mahala pema, Na waliokuwa wagonjwa Mungu awape afya njema na tumwombe Mungu kwa kila lililokuwa zitokwa mwaka uliopita,atufanyie wepesi katika mwaka huu mpya wa 2013
 
Gerald Joseph: Heri ya mwaka mpya mdau wa Standard Radio pamoja na wafanyakazi wote wa Standard Radio
Tusifikirie yaliyopita maana yanaumiza moyo,wala tusifikirie yajayo maana yanakatisha tamaa.Tufikirie yaliyopo na kuyafanyia kazi
 
 
Khadija Mahamba: Tumshukuru Mungu kwa kutupa nafasi tena ya kuendelea kuwepo duniani 2013 haimaanishi ambao hawajauona mwaka huu Mungu hawapendi La! Ila jiulizze utafanya yale aliyoyaagiza uyafanye hapa duniani? Namaanisha Badilika, rudi kwa Muumba wako achana na mabaya yaliyokuwa yakikupendeza fanya mazuri yampendezayo Muumba wako na wazazi wako . Endelea kusikiliza Standard radio
 
Elizabeth Mwaja: Heri ya mwaka mpya 2013, Kufika mwaka 2013 ni uweza wake Mwenyezi Mungu kwani wengi walitamani kufika lakini hawakuweza kufika kutokana na vikwazo mbalimbali kama vile maradhi, vita na ajali. Tumwombe Mungu atuvushe tena mwaka huu
 
Agnes Samweli: Namshukuru Mungu amekuwa mwema kwa Standard Radio kwani changamoto tulizokutana nazo,hatujutii, ni hali ya kawaida, hivyo nawaomba wana Standard wote tushirikiane kwa upendo wa dhati ili tuweze kusonga mbele
 
Deborah Marco: Kila mtu yupo duniani kwa makusudi kamili ya Mungu.Nawatakia mafanikio mema ya mwaka 2013 yale yote ambayo hujayatimiza 2012 uyatimize 2013
 
Joseph Monko, Nawashukuru wafanyakazi wote wa standard Radio kwa moyo tuliouonesha, tuendelee kwa moyo huohuo. nawatakia heri ya mwaka mpya
 
 
 
 
Noel Exavery: Furahini katika Bwana siku zote tena nasema furahini, upole wenu na ujulikane na watu wote
 
 
 
 
 
 
 

1 comment:

Unknown said...

Kila la kheri katika kuwahabarisha wanasingida. 2013 iwe tofauti na mwaka jana kwa uhalisia wa programs na content. Viva Singida