Monday, January 21, 2013

KITUO CHA MABASI UBUNGO CHALETA BALAA


Watu watatu wamejeruhiwa  na magari ishirini na manne kuharibika baada ya ukuta wa kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo jijini Dar es salaam  kuanguka leo asubuhi katika eneo la kuegeshea magari.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kinondoni Bw. Charles Kenyela amesema ukuta hbuo umeanguka kufuatia kazi ya ubomoaji inayoendelea katika eneo hilo. Amesema watu waliojeruhiwa wamepelekwa hospitali kupata matibabu.
Kufuatia ajali hiyo watu wametakiwa kuwa waangalifu katika eneo la kituo cha mabasi Ubungo, ili kuepuka athari zinazoweza kutokea wakati zoezi la kuondoa magari yaliyoangukiwa na ukuta, likifanyika

No comments: