Monday, January 21, 2013

CHADEMA WAWALALAMIKIA WANAWAKE


Mratibu wa sera za chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoani Singida Bi Jesca Kishuwa amelalamikia baadhi ya   wanawake mkoani Singida kutohudhuria  katika mikutano ya hadhara  hasa ya kisiasa.

 

Bi Jesca amesema hayo jana wakati wa mkutano wa hadhara wa  chama cha Democrasia na Maendeleo (CHADEMA) uliofanyika katika viwanja vya stendi ya zamani ya mabasi mkoani Singida.

 

Bi Jesca ameeleza kuwa licha ya idadi kubwa ya watanzania kuwa na kundi kubwa la wanawake, bado akina mama wako nyuma kimaendeleo na kiufahamu kutokana na kutojihusisha na masuaala ya kisiasa

No comments: