Monday, July 29, 2013

CHF YAKUSANYA ZAIDI YA MILIONI 377 IRAMBA


Na:Mwandishi wetu
Wilaya ya Iramba mkoani Singida, imekusanya zaidi ya shilingi milioni 377  zikiwa ni makusanyo ya ada za uanachama wa mfuko wa afya ya jamii (CHF), tangu mfuko huo uanzishwe juni mwaka 1998 hadi sasa.

 
Hayo yamesemwa mwishoni mwa wiki na mkuu wa wilaya hiyo, Yahaya Nawanda, wakati akizungumza na  waandishi wa habari ofisini kwake juu ya maendeleo ya mfuko huo, ambao umekuwa mkombozi mkubwa kiafya kwa wakazi wa wilaya hiyo.

 
Amesema kiasi hicho cha fedha, ni ada za wakazi wa kaya 37,710 wa wilaya hiyo  zilizojiunga na mfuko huo ambayo ni sawa na zaidi ya aslimia 50 za kaya 78,000 za wilaya ya Iramba.

 
Mkuu huyo wa wilaya, amesema licha ya fedha hizo kugharamia matibabu kwa wanachama, pia zimetumika katika kukarabati majengo ya vituo vya huduma za afya na nyumba za kuishi watumishi.

No comments: