Tuesday, July 16, 2013

VIJANA WAMEONYESHA CHANGAMOTO KUBWA YA MAENDELEO ENDAPO WATAGOMBEA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI NCHINI


Na;Muss Mbeho
Vijana wa manispaa ya singida  wametakiwa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi,  hasa kwa kipindi kijacho cha uchaguzi mkuu  ili kuleta changamoto za maendeleo kwa taifa.

Hayo yamesemwa leo na mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Singida Bw. Ibrahimu Kijanga wakati  akizungumza  na Standard Radio ofisini kwake kuhusu uwajibikaji wa vijana katika suala la uongozi.

 
Bw.  Kijanga amesema vijana wamepewa nafasi mbalimbali za uongozi katika jumuiya zao, kwa  lengo la kuwaandaa vijana kuwa viongozi wachapa kazi kwa sasa na kwa wakati ujao, katika sekta za serikali na sekta binafsi.

 
Aidha, Bw.  Kijanga amewataka vijana kutojiunga na makundi mabaya na kuepuka kutumika vibaya kama vile kushiriki maandamano ambayo si halali kisheria,  na badala yake wafanye kazi kwa bidii ili kupiga vita umasikini.

 

 

 

No comments: