Tuesday, July 16, 2013

WANANCHI MKOANI SINGIDA WAHIMIZWA KUHIFADHI CHAKULA




Na. Edilitruda chami

Wananchi mkoani singida wametakiwa kujifunza mbinu mbadala za  kusindika vyakula ili kuvihifadhi kwa matumizi ya baadae na kuepukana na njaa ambayo inaweza kujitokeza.

Akizungumza na standard radio meneja wa viwanda vidogovidogo SIDO mkoani Singida  Bi. Shoma Kibende amesema  endapo  wananchi watatumia mbinu za kuhifadhi vyakula na hata kufungasha kwa njia ambayo ni salama hapatakuwepo na upungufu wa vyakula.  

Amesema mkoa wa Singida unazalisha vyakula vingi kama vile  nyanya, matunda, mbogamboga, karanga  lakini vinaharibika mapema kutokana na watu kutojua njia sahihi za kuhifadhi vyakula kwa matumizi ya baadaye.

Aidha, amesema Sido ina mpango wa kuhakikisha mwananchi anajikita katika shughuli za kijasiriamali  kwa kutoa mafunzo mbalimbali ili kuongeza kipato chao  binafsi na kuongeza thamani ya bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali pamoja na kujifunza mbinu za usindikaji. 

Jumla ya viwanda 76 vimefikiwa na SIDO katika kutoa mafunzo ya ujasiriamali na usindikaji bora wa vyakula na matunda, kama njia pekee ya kutokomeza njaa kwa siku za baadae

No comments: