Monday, July 22, 2013

MAABARA SHULENI ZINAONGEZA WASOMI


Na:Prisca Rojin
Wakazi wa  kata ya Mandewa mkoani Singida wameombwa kushiriki vyema katika ujenzi wa maabara ili kuongeza idadi ya wasomi nchini.

 
Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa kitongoji kata ya Mandewa, Bw. Juma Assi wakati akizungumzia hatua iliyofikiwa sasa katika ujenzi huo wa maabara.

 
Bw. Assi amewaomba watu wote wenye uwezo wa kufanya kazi kushiriki pamoja ili kupanua wigo wa elimu kwa vizazi vilivyopo na vijavyo ili kupunguza idadi ya watu wasiojua kusoma wala kuandika.

 
Aidha, amewashukuru baadhi ya wakazi ambao wanaonesha kujitoa kwa hali na mali na kuwataka wengine kuiga mfano huo ili kuendeleza kata ya Mandewa katika sekta ya elimu.  

 
 
 

No comments: