Tuesday, July 16, 2013

MGOGORO WA MPAKA WA ZIWA NYASA BADO UZI NI ULEULE KWA RAIS JOYCE BANDA



Na:Iran radio


Rais Joyce Banda wa Malawi amesema kuwa nchi yake haina nia ya kulegeza kamba katika mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na Tanzania.

 
Kiongozi huyo ametoa msimamo huo baada ya kukutana na marais wa zamani Bw. Joachim Chissano wa Msumbiji na Bw. Thabo Mbeki wa Afrika Kusini ambao ni wajumbe maalum wa jumuiya ya SADC katika mgogoro huo.

 
Rais Joyce Banda amesema madai ya Tanzania kwamba inamiliki sehemu fulani ya Ziwa Nyasa si ya kweli na kwamba mpaka uko ufukweni mwa ziwa hilo.

 
Amesema nchi yake inafuatilia kwa karibu upatanishi wa SADC na kwamba isiporidhishwa na maamuzi ya jumuiya hiyo italiwasilisha suala hilo mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu ICJ.

 
Joachim Chissano na Thabo Mbeki wanatarajiwa kuelekea Tanzania na kukutana na Rais Jakaya Kikwete ili kujadili mgogoro. Tanzania inasisitiza kwamba mpaka wake na Malawi uko ndani kabisa ya Ziwa Nyasa. 

No comments: