Tuesday, July 16, 2013

MAHAKAMA MKOANI SINGIDA YAFUTA KESI YA UTAPELI


Na MAZIKU MOTTO

 

Kesi iliyokuwa inamkabili Bw. Abdallah Ramadhani mkazi wa Puma manispaa ya Singida imefutwa na mahakama ya mwanzo Utemini kutokana na mlalamikaji Rajabu Ramadhan pamoja na mshtakiwa kushindwa kufika mahakamani.

 

Hukumu hiyo imetolewa na hakimu wa mahakama hiyo Bw Simon Njau, ambapo amesema mnamo tarehe 24 june mwaka huu, mshitakiwa Bw Ramadhan alikaidi wito uliotolewa na mahakama uliomtaka afike mahakamani hapo.

 

Bw Njau amesema kwa kitendo cha kukaidi wito wa mahakama ni kosa na ni kinyume cha sheria za nchi.

 

Mahakama hiyo imeamua kuondoa shauri hilo kutokana na mlalamikaji kushindwa kufika mahakamani ili atoe ushahidi juu ya tuhuma zinazomkabili Bw Ramadhan.





No comments: