Tuesday, July 16, 2013

UMASKINI NI CHANGAMOTO KWA MAENDELEO YA BURUNDI




Na Iran Radio


Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa  kuisaidia nchi hiyo katika juhudi za kupunguza umasikini na changamoto zinazoikabili.

Wito huo ametolewa jana katika ufunguzi wa mkutano wa ufuatiliaji wa wafadhili wa Burundi ambao unafanyika kwa siku mbili mjini Geneva, Uswisi.

Aidha Rais huyo amewapongeza washirika kwa uungaji mkono na kusema kuwa tangu mwaka 2005 nchi ya Burundi  imepata maendeleo makubwa katika sekta mbalimbali, zikiwemo utawala bora, amani na usalama, masuala ya hali ya hewa, elimu, afya na miundo mbinu.

Ametaja changamoto mbalimbali zinazoikabili nchi hiyo kuwa ni pamoja na  migogoro ya ardhi, ukuaji mdogo wa uchumi, utapiamlo, kilimo cha kisasa, ongezeko la kasi la idadi ya watu, ukosefu wa nishati pamoja  na mabadiliko kwenye sekta ya elimu.

Amesema nchi hiyo inahitaji kusaidiwa kuandaa uchaguzi ulio huru na  wa haki na utakaoshirikisha watu.

No comments: