Monday, July 22, 2013

TANZANIA NA CHINA KUENDELEZA USHIRIKIANO



Na:mwandishi wetu
Rais Jakaya Kikwete amekutana na ujumbe wa China unaoongozwa na mkurugenzi wa Idara ya ukaguzi wa mahesabu ya China Bw. Liu Jiayi.

Katika mazungumzo na uju mbe huo,  rais Kikwete amesema katika miaka ya hivi karibuni, mawasiliano ya ngazi ya juu na ya umma kati ya pande hizo mbili yamekuwa yakiimarishwa.

Viongozi wa China wametembelea Tanzania, na kusaini makubaliano ya ushirikiano na kutoa msaada na uungaji mkono mkubwa kwa Tanzania. Rais Kikwete ametoa shukurani kwa uungaji mkono unaotolewa na China kwa kazi ya idara ya ukaguzi wa mahesabu ya Tanzania, na kuelezea matumaini yake kuwa,  Idara ya ukaguzi wa mahesabu ya China itatoa uungaji mkono na msaada kwa wingi zaidi katika kutoa mafunzo kwa wataalamu, na kubadilishana uzoefu.

 
Bw. Liu Jiayi amesema Idara ya ukaguzi wa mahesabu ya China itafanya juhudi kadri iwezavyo kuhimiza ushirikiano wa fedha na miradi kati ya nchi hizo mbili.

No comments: