Wednesday, July 17, 2013

RAIS ABDELAZIZ BOUTEFLIKA AREJEA NCHINI KWAKEWA ALGERIA BAADA YA KUPATA MATIBABU NCHINI UFARANSA


 
 
Na:Iran Radio
Habari kutoka Ufaransa zinasema, Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria amerejea nchini kwake baada ya kupata matibabu nchini Ufaransa.

 

Habari zinasema kuwa, Rais Bouteflika ameondoka nchini Ufaransa jana kuelekea nchini kwake. Rais huyo mwenye umri wa miaka 76 alipelekwa nchini Ufaransa baada ya kukumbwa na ugonjwa wa kiharusi mwishoni wa mwezi Februari ambapo awali alilazwa katika hospitali ya kijeshi ya Valde Grace na kupelekwa katika hospitali nyingine ya mjini Paris, Ufaransa.

 

Kutokuwepo kwake kisiasa nchini Algeria, kuliibua maswali mengi hasa kuhusiana na nafasi ya uraisi nchini humo. Hali hiyo ilivifanya vyama na makundi ya kisiasa yanayoipinga serikali inayoongozwa na Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria, vilitaka kufanyika uchaguzi kabla ya wakati kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo, kutokana na kuugua rais huyo.

 

No comments: