Wednesday, July 17, 2013

MADIWANI WAGOMA KUSHIRIKI UCHAGUZI WILAYANI BUHIGWE MKOANI KIGOMA


 
 Na:Mwandishi wetu
 Madiwani watano wa Chama Cha Mapinduzi wilayani Buhigwe Mkoani Kigoma, wamesema hawatoshiriki uchaguzi wa kumpata mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, kutokana na ukiukwaji wa sheria uliofanyika.

Madiwani hao wametoa kauli hiyo kufuatia uchaguzi wa jina la atakaekuwa mgombea wa kiti hicho uliofanyika juzi wilayani humo kupitia chama hicho kudaiwa kufanyika kinyume na utaratibu.

Madiwani hao wamesema katika uchaguzi wa nafasi hiyo kupitia CCM zilitangazwa nafasi nne pamoja na kutakiwa kuwa na majina matatu ya wagombea lakini yalitangazwa majina mawili pamoja na nafasi 2 kitu ambacho ni kinyume na  kanuni za chama hicho

Mmoja wa madiwani hao Bw Alois Edward diwani wa kata ya Biharu amesema baada ya tukio hilo baadhi ya madiwani walihoji na hawakupata majibu kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi huo zaidi ya kutishiwa kupokonywa nafasi zao pamoja na kadi za uanachama ambapo wamesusia uchaguzi huo
.
Standard Radio imemtafuta katibu wa chama hicho mkoa wa kigoma Bw Mohammed  Nyawenga msimamizi wa uchaguzi huo, ili kuzungumzia tukio hilo na kudai kuwa hayupo tayari kuzungumza lolote na hata alipotafutwa kwa njia ya simu haikupokelewa.

No comments: