Wednesday, July 17, 2013

MUUNGANO WA KAMPUNI ZA ULINZI NA JESHI LA POLISI KUTAIMARISHA UFANISI KATIKA KAZI


Na:Jonhson Soah
 
Kampuni binafsi za ulinzi mkoani singida zimeshauriwa kuimarisha ushirikiano na jeshi la polisi ili kuleta ufanisi.

 
Hayo yamesemwa leo na kamanda wa polisi mkoa wa Singida, ACP Geoffrey Kamwela wakati wa kikao na kampuni binafsi za ulinzi ofisini kwake, kwa lengo la kubadilishana taarifa juu ya usalama mkoani hapa.

 
Kamanda kamwela ameyataja mambo waliyokubaliana kuwa ni utaratibu wa kuendesha mafunzo ya darasani pamoja na ukakamavu kwa walinzi binafsi yatatolewa na jeshi la polisi.

 
Aidha Bw. Kamwela amezitaka kampuni binafsi kuajiri watu kulingana na uadilifu, na umri unaostahili na kuzishauri kampuni hizo zipitie jeshi la polisi ili kuhakikishiwa taarifa sahihi za waajiriwa.

 
Mkoa wa Sngida una kampuni za ulizni binafsi zipatazo 18 zilizosajiliwa kisheia.

No comments: