Monday, July 29, 2013

VYOMBO VYA DOLA KUSAIDIA WATOTO WAISHIO MAZINGIRA HATARISHI


Na:Mussa Mbeho
Wakazi wa mkoa wa singida wameshauriwa  kutoa taarifa kwenye  vyombo vya dola pindi wanapobaini kuwa kuna watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi ili kuwasaidia.

Hayo yamesemwa na Afisa ustawi wa jamii wa mkoa wa singida Bi. Zuhura Karya  wakati akikabidhi watoto  waliogundulika wakiishi katika mazingira magumu kwa uongozi wa shule ya msingi St.Vicent  iliyopo Itigi wilayani Manyoni.

Bi. Karya amesema kuwa wananchi washirikiane na viongozi wa serikali ili kufichua watoto ambao wanaishi katika mazingira hatarishi ili kuwawezesha watoto kupata haki zao za msingi na si kuwaacha waendeleee kuteseka.

 

Aidha amesema kuwa wataendelea  kuwasaidia watoto ambao wanaoteseka kwa kuwalea na kuwasomesha ili kuondokana na tatizo la ongezeko la watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

Bi. Karya amewataja watoto waliopatikana katika mazingira hatarishi kuwa ni Juma Masunga mwenye umri wa miaka 13, Swalehe Masunga mwenye umri wa miaka 11, Rajabu Masunga mwenye umri wa miaka 8, na Tabu Masunga mwenye umri wa miaka 6 ambao walikuwa wakiishi na baba yao aliyekuwa akijulikana kama mganga wa jadi kumbe ana matatizo ya akili.

 

No comments: