Monday, July 22, 2013

VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI NI UKOMBOZI WA UCHUMI


 
Na:Edilitruda Chami
Wakazi wa mkoa wa Singida wameaswa kutotegemea ajira kutoka mashirika binafsi na serikalini badala yake kujiunga  na kuanzisha vikundi mbalimbali vya kijasiriamali ili kujikomboa kiuchumi.

Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa mradi wa mafunzo woman society  mkoani singida bi. Amina Abubakari   wakati akizungumza na standard radio juu ya umuhimu wa kuunda makundi ya kijasiriamali kwa wanawake katika kujiendeleza kibiashara.

Bi. Amina amesema  lengo la mradi huo ni kuhakikisha  maambukizi ya virusi vya ukimwi hayaenei kwa kuwawezesha   wanawake kuwajibikaji na shughuli za kiuchumi, kuzuia ongezeko la  mimba za utotoni, pamoja na  kuwaweka walemavu na watoto wanaoishi katika mazingira magumu  katika hali nzuri ya maisha kwa kuwajengea uwezo wa kujiajiri wenyewe.

Amesema  kila mwananchi atambue umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu kwa kuwashirikisha wananchi wengine katika miradi mbalimbali ya kimaendeleo, bila kubaguana kwa misingi ya dini, siasa au kabila.  Mradi wa mafunzo woman society  umeanziasha vikundi vya wajasiriamali wadogo wadogo 15 wanaoshughulika na kilimo, ufugaji na usindikaji wa vyakula, na wameweza kutoa mafunzo kwa vijana 273.

No comments: