Monday, July 29, 2013

SERIKALI NA DINI ZINAFANYA KAZI MOJA KATIKA HUDUMA ZA JAMII


Na;Mwandishi wetu
Mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone amesema serikali na dini zinafanya kazi moja ya kumhudumia mwananchi katika nyanja mbali mbali za huduma za jamii.

 
Dk. Kone amesema hayo mwishoni mwa wiki katika sherehe za kuwekwa wakfu askofu Benjamin Yared Wellya wa Kanisa la Tanganyika African Church TAC zilizofanyika katika kijiji cha Chikuyu wilayani Manyoni.

 
Amesema serikali mkoani Singida mikakati ya kanisa la TAC katika kupambana na umaskini, kulinda amani na kuwa na mipango ya kuanzisha taasisi za elimu na afya katika eneo la Chikuyu.

 
Aidha, amewataka waumini kufanya kazi kwa juhudi na maarifa kwa kuzingatia utaalam wa washauri wa kilimo. Dk. Kone ametoa wito kwa wakazi wa mkoa wa Singida kutumia fursa nyingi zilizopo ili kuondokana na umaskini.

 
Awali Askofu Benjamin Yared Wellya, ameahidi kushirikiana na waumini wote, serikali na taasisi nyingine katika kulinda amani, upendo na mshikamano katika jamii.

No comments: