Tuesday, July 23, 2013

UTAMADUNI WA KITANZANIA HUENDANA NA MAADILI MAZURI


 
Na:mussa mbeho
 
Vijana katika Manispaa ya Singida wameshauriwa kufuata maadili mazuri ili kuendeleza utamaduni wa  makabila yao.

 
Kauli hiyo imetolewa  leo  na Afisa utamaduni wa manispaa ya singida Bw. Anacletus Mkuki wakati akizugumza na  Standard Radio.  Amesema endapo vijana watafuata utamaduni wa makabila yao itasaidia kupunguza  tatizo la mmomonyoko wa maadili uliopo hivi sasa.

 
Bw.  Mkuki amesema kuwa  vijana wengi wamesahau maadili ya makabila yao kitendo ambacho  kinasababisha wengi wao kutokuwa na  maadili mema.

 
Aidha, Bw. Mkuki amewaasa vijana wote kuzingatia mila na desturi zao ili kuepukana na mmomonyoko wa maadili uliopo mkoani Singida.

 

 

No comments: