Wednesday, July 17, 2013

AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUKUTWA NA NYARA ZA SERIKALI MKOANI SINGIDA


Na;Fatma Munah
 
Mkazi  mmoja wa kijiji cha Misughaa mkoani Singida amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi wilaya  kwa kosa la kukutwa na nyara za serikali  kinyume cha sheria ya wanyama pori.

 
Akisomewa  mashtaka,   mshtakiwa  Bw Andrea Patric,  mwendesha mashtaka wa serikali sajent Lawrence mbele ya hakimu Bi Terrysoph Tesha  amesema  mshtakiwa  alikutwa na nyara za serikali tarehe 09 mwezi July mwaka 2012 majira ya saa kumi na nusu jioni katika kijiji cha Misughaa wilaya na mkoa wa Singida

 
Aidha sajent Lawrence amesema mshtakiwa alikutwa na kilo moja na nusu ya nyama ya digidigi ambayo thamani yake ni shilingi laki nne na elfu ishirini na tano ikiwa ni mali ya serikali.  

 
Mshtakiwa amekiri kosa na mahakama imemtia hatiani na kumhukumu kwenda jela kwa miezi mitatu au kulipa faini ya shilingi elfu hamsini, kama onyo kwa kuwa mshtakiwa ni mara yake ya kwanza kutenda kosa hilo.

No comments: