Tuesday, July 16, 2013

NCHI YA KENYA NA NIGERIA ZIMEONYESHA USHIRIKIANO WA KUPANUA WIGO WA KIBIASHARA


Na:Iran Radio
Serikali za Kenya na Nigeria zimekubaliana kupanua wigo wa ushirikiano katika sekta mbalimbali hususan biashara.

Hayo yamebainika kwenye mkutano kati ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na mwenzake Goodluck Jonathan wa Nigeria mjini Abuja. Viongozi hao wamesisitiza umuhimu  wa kuimarishwa biashara miongoni mwa nchi za Afrika huku Rais Kenyatta akisema sera za nje za serikali yake zitazingatia zaidi biashara na nchi za Kiafrika.

Rais Jonathan kwa upande wake amesema bunge la nchi yake litajadili njia za kupunguza urasimu ili kurahisisha biashara na Kenya. Rais Kenyatta yuko nchini Nigeria kuhudhuria mkutano maalum wa Umoja wa Afrika wa kujadili jinsi ya kupunguza maambukizi ya virusi vya HIV na ugonjwa wa Kifua Kikuu barani Afrika.

Mikataba ya ushirikiano kati ya nchi na nchi, inatarajiwa kusainiwa wakati marais wa nchi mbalimbali watakapokutana baada ya mkutano huo.

 

No comments: