Wednesday, July 17, 2013

KUUZA NYARA ZA SERIKALI KWA MASLAHI BINAFSI NI KOSA KISHERIA


 
Na;Prisca Rojin
 
Afisa mhifadhi wa wanyamapori halmashauri ya wilaya ya Singida Bw. Augustino Lorry,  amewataka wananchi kutoa taarifa pale inapogundulika mtu ameuza nyara za serikali kwa maslahi yake binafsi,  ili achukuliwe hatua za kisheria.

 
Kauli hiyo inafuatia mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Hassan Jumannne mkazi wa mtaa wa Mamtanda Mandewa, anayetuhumiwa na wakazi wenzake kuhamisha maji kutoka  kwenye bwawa linalotumiwa na wakazi wa eneo hilo na kuuza vyura.

 
Afisa mhifadhi wa wanyamapori Bw. Lorry, amesema  kuwa mtu huyo amevunja sheria ya uhifadhi wa wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009 ya kuuza nyara za serikali bila kibali.

 
Aidha Bw Lorry ametoa tahadhali kwa jamii nzima kulinda na kutunza wanyama pia kutouza nyara za serikali bila kibali kutoka kwa maafisa wa wanyamapori.

 

 

No comments: