Tuesday, September 10, 2013

WANANCHI WAASWA KUTOKUBURUZWA KATIKA KATIBA MPYA

Na;Edson Raymond
wananchi wameaswa kutokubali kuburuzwa na mawazo yanayotolewa na vyama vya siasa, katika mchakato wa kupata katiba mpya, bali kuzingatia mahitaji ya umma kwa maendeleo ya taifa.

wito huo umetolewa leo na baadhi ya viongozi wa vyama vya ccm na chadema wakati wakizungumza na standard radio, kuhusiana na mchakato wa kupata katiba mpya.

katibu mwenezi wa ccm mkoa wa singida mwl. musa sima, amesema kuwa kwa sasa hali ilivyo vyama vya siasa, vinazingatia propaganda za kisiasa ambazo kimsingi zinaegemea kwenye mahitaji ya chama, kuliko kuegemea katika mahitaji ya jamii, jambo ambalo ni hatari katika mustakabali wa maendeleo katika taifa hili.

 

kwa upande wake katibu mwenezi wa chadema mkoa wa singida mwl. mutta anselim, amesema kuwa nafasi ya chama cha siasa katika mchakato wa katiba mpya, ni kutoa elimu kwa wananchi, hivyo wananchi wanatakiwa kupima elimu hiyo, kama inatija kwao ama la.

aidha wametoa wito kwa wananchi kusubiri hatua ya mwisho ya kupiga kura ya maoni, katika rasimu itakayopitishwa na bunge maalum la katiba, kama itakuwa na mambo wanayoyahitaji ama vinginevyo,  ili kupata katiba inayokidhi mahitaji ya wananchi.

No comments: