Tuesday, September 10, 2013

RWANDA YAONGEZA USHURU DHIDI YA MAGARI YA MIZIGO YA TANZANIA

Na;mwandishi wetu
madereva wa malori kutoka nchini wamepata usumbufu kuingia rwanda kabla ya kuanza kutumika kwa ushuru mpya, wa barabara ambao umeanza kutumika tena leo, kwa upande wa rwanda ukilenga magari kutoka tanzania tu.

rwanda iliongeza ushuru kwa zaidi asilimia  229, dhidi ya magari ya mizigo ya tanzania tu kutoka viwango vya zamani vya dola za marekani 152, hadi dola 500 kwa madai ya kutaka usawa na tanzania.

ushuru huo ambao ulianza kutumika rasmi septemba mosi mwaka huu, kisha kusitishwa kwa muda, ulitarajiwa kurejeshwa tena leo kulingana na tangazo la rwanda mpakani rusumo.

mkuu wa wilaya ya ngara, bw. constantine kanyasu, amethibitisha serikali ya rwanda kuongeza ushuru wa barabara kutoka dola 152, hadi dola 500 na kwamba baada ya mazungumzo na serikali ya tanzania,  walikubali kurejesha kiwango cha zamani, lakini kwa muda tu.

No comments: