Wednesday, September 25, 2013

MKUU WA MKOA WA SINGIDA AWATAKA WAKULIMA KUTUNZA ZIADA YA CHAKULA.



 Na;Boniface Mpagape
 Mkuu wa mkoa wa singida Dr parseko Kone amewataka wakulima mkoani humo  kutunza ziada ya chakula kilichopatikana katika mavuno ya msimu huu
Kauli hiyo imetolewa leo katiaka kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa katika ukumbi wa Veta mjini Singida
Dr Kone amestoa kauli hiyo baada ya kusomewa taarifa ya utekelezaji wa sekta  ya kilimo ambayo imeonyesha kuna kuna tani zaidi ya laki nne za ziada katika msimu huu
Taarifa hiyo imesema kuwa bado kuna changamoto ya matumizi ya jembe la la mkono na idara husika inafanbya juhudi za kuelimisha wakulima kutumia teknolojia za kisasa katika kuongeza uzalishaji

No comments: