Tuesday, September 10, 2013

WANAFUNZI WA DARASA LA SABA KUANZA MITIHANI KESHO

Na;Mwandishi wetu
jumla ya wanafunzi laki nane na sitini na nane elfu na thelathini wa darasa la saba nchini, wanatarajia kufanya mtihani wa kuhitimu elimu yao ya msingi kesho. 

naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi, philipo mulugo, amesema kuwa, mtihani huo utakaojumlisha masomo matano, utafanyika kwa siku mbili kuanzia kesho hadi kesho kutwa alhamisi.

kati ya idadi hiyo ya wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani huo, wavulana ni laki nne na elfu kumi na mbili na mia moja na tano, sawa na asilimia 47, na wasichana laki nne na elfu hamsini na tano na mia tisa ishirini na tano, sawa na asilimia 52.52. jumla ya masomo matano yanatarajiwa kutahiniwa na wanafunzi hao ambayo ni pamoja na kiswahili, kiingereza, sayansi, hisabati na maarifa ya jamii.


aidha, waziri mulugo pia amewataka wasimamizi  kusimamia kwa umakini na uadilifu, pamoja na kuwaasa wanafunzi wote kutojihusisha na vitendo vyovyote vya udanganyifu wa mtihani, kwani watakaobainika kufanya hivyo watafutiwa matokeo yao yote ya mtihani.

No comments: