Wednesday, September 25, 2013

WAKULIMA ELFU 10 NA MIA5 KUNUFAIKA NA MRADI WA UWEZESHAJI WA FAMILIA NCHINI




Na.Mwanishi wetu

Jumla ya wakulima elfu 10 na mia 5 kutoka mikoa 15 hapa nchini wanatarajiwa kunufaika na mradi wa uwezeshaji wa familia kupitia maendeleo ya kilimo uliofadhiliwa na Bangladesh kupitia taasisi ya BRAC

Akiongea na waandishi wa habari mratibu wa mradi huo kanda ya Ziwa Bw George Zabron amesema mradi huo umeanza mwezi wa April mwaka huu ambapo kila mkulima atapatiwa mtaji kwa mwaka wa kwanza wa EURO 84
Amesema mradi huo umelenga kuleta uzalishaji kwa mkulima ambapo watajikita na ufugaji wa kuku wa kienyeji na mkulima anayelima mahindi kuanzia nusu ekari
Bw Zabron ameongeza kuwa kila mkulima atakuwa anapewa pembejeo kwa lengo la kuthibiti matumizi yasiyokuwa sahihi ya mradi huo

No comments: