Tuesday, October 23, 2012

WANAHABARI SINGIDA WANOLEWA

Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa makni kumsikiliza mwezeshaji katika mafunzo ya sera na ufuatilaji wa bajeti ukumbi wa social training centre manispaa ya singida
 
NA, Doris Meghji

Singida

Elimu ndogo ya uchambuzi wa sera miongoni wa waandishi wa habari nchini ni sababu kuu mojawapo inanyopelekea kutohabarisha umma juu ya mambo mbali mbali ya maendeleo imefahamika.

Hayo yamebainika leo mkoani Singida kwa waandishi wa habari mkoa wa singida katika mafunzo uchambuzi wa sera na ufuatiliaji wa bajeti(policy analysis and budget tracking) yaliyoandaliwa na Muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania(UTPC) kwa waandishi wa habari wa mkoa huu.

Akiongea na Standard Radio Mwezeshaji wa mafunzo hayo Bwana Adam Ndokeji toka mwanza amewataka waandishi wa habari kubadilika kwa kufanya uchambuzi wa sera mbali mbali za masuala ya maendeleo lengo likiwa ni kuuhabarisha umma kwa mambo ya kimaendeleo.


Naye mmoja wa waandishi wa habari wa mkoa wa singida Bi Awila Silla anasema “nimefurahia sana mafunzo hayo ingawa yamechelewa kujifunza kwani tayari tulishavirunda kuripoti mambo mengi ya maendeleo katika umakini na umahususi unaotakiwa,hata hivyo ni wakati muufaka sasa wa mtazamo chanya kuahidi kuwa elimu ya mafunzo haya itaondoa mapungufu yote ya nyuma”amesisitiza Bi silla.

Katika mafunzo hayo jumla ya waandishi kumi na nane(18) wanapatiwa mafunzo hayo mkoani singida yatakayodumu kwa kipindi cha siku nne.

No comments: