Friday, October 5, 2012

AJALI MBAYA IRAMBA YAUA WATOTO

NA  Phesthow  sanga

Ajali  mbaya iliyotokea  Usiku wa  Kuamkia  oct 03 Mwaka  huu  katika  Kijiji  Cha Malendi  Tarafa  ya Shelui  Wilayani  Iramba  Mkoani  Singida na kuwa  Watu watatu.
Watu  Waliofariki Dunia papo hapo  Walifahamika  kuwa  ni  Suleiman  Kaberege { 21} Mhehe  Mkazi  Wa  Igunga  Mkoani Tabora  Wengine  ni  Mwanamke   aliyefahamika  Kwa  jina  moja  la  Mwanaid   Pamoja  na  Mtoto  Wake  Ambaye  hakuweza  Kufahamiaka  jina  mara moja.
Akiongea  na  Wanahabari  Katika Hospitali ya Wilaya  ya  Iramba  jana  Matron  wa  hospitali hiyo Bi ,Perpetua  Mnkumbo   alisema  Kuwa, Usiku wa saa sita kuamkia Oct 3  walipokea miili ya marehemu  Watatu  na Majeruhi Ishirini na saba  27 na Baadaye wawili  Walifariki Dunia wakati  madaktari na manesi wakiendelea kuwahudumia.
Aidha Aliwataja  Waliofariki  Hospitalini  hapo  kuwa  ni  Pamoja   na  Nana  kulwa{ 16}  na  Erasto Willimu {39},alisema  kuwa  Majeruhi  Wengine  Waliweza  Kupewa   Rufaa  ya  kwenda  Hospitali   kubwa  kwa   Matibabu  Zaidi,  Kutokana  na kuendelea kutoka damu mdomoni.
Akielezea  Chanzo  Cha  ajali  hiyo   Jumapili  Elia{ 43} Ambaye  ni  Mhanga   wa  Ajali  Alisema  kuwa  Gari hilo   halikuwa  na Taa
Kutokana  na   kukithiri  kwa  Ajali  Nyingi  Barabarani  Wananchi  Walioshuhudia  Ajali  hiyo  Mbaya Wamelishauri  Jeshi   la  Polisi  Nchini  Hasa  Askari  wa  Usalama   Barabarani  kuwa  Makini na  Madereva   Wazembe  na  wasiozingatia  Sheria  za  barabarani,  Polisi  Wilayani  hapa  Wamethibitisha  Kutokea   Kwa  Ajali  hiyo   na  juhudi   za  Kumutafuta   Dereva  Wa  gari  hilo  Zinaendelea .
       Jeshi la polisi mkoani Singida limekiri kutokea kwa ajali hiyo


No comments: