Sunday, October 14, 2012

MBIO ZA BAISKELI SHINYANGA


Na edilitruda chami
Mkoa wa shinyanga umeendelea  kushamiri katika mashindano ya mbio za  baiskeli ambapo  chama cha wapanda biskeli katika wilaya ya shinyanga  vijijini {CHABASHI} kimeweza kuandaa mashindano ya umbali wa kilomita 35  kutoka  kijiji cha Itwangi kwenda Puni kwa kilomita 20 na kutoka itwang kwenda kituli kwa kilomita 15 ambapo washiriki  26 walijitokeza katika mbio hizo.
Juma Tagara  ndiye aliyeibuka mshindi wa kwanza, na  akazawadiwa  taslim sh. laki moja akifuatiwa na masingija ndumrli ayeliweza  kuibuka na taslim shilingi elfu sabini na mshindi wa tatu alikuwa ni Charles Clement aliejinyakulia kitita cha sh. elfu hamsini zilizotolewa na  mdhamini wa mbio hizo  Senge  Sesaguli.
Katibu wa chama cha mbio za Baiskeli wilaya ya shinyanga vijijini Shija Dalali amesema kuwa lengo la kugawa zawadi hizo kwa washindi katika mashindano hayo ni kuhamasisha vijana kushiriki katika mashindano mbalimbali  na kuhakikisha kuwa wanaibua vipaji vya wanamichezo  watakaoshiriki katika ligi mbali mbali. vijijini                                                                                                                                             
Mbali na mbio za baiskeli mkoa huo unaendesha mashindano  mbalimbali  ambapo zawadi za vitu halisi hutolewa kama vile ngombe mnyama, mbuzi mnyama, mpira wa miguu na pamoja na fedha ambazo zimekuwa zikitolewa na wadhamini mbalimbali.

No comments: