Wednesday, October 10, 2012

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE 2012 ABAINI UOZO SERIKALINI


Na. Abdul BANDOLA
Kiongozi wa mbio  za mwange wa uhuru wa Tanzania mwaka huu  Kapteni Honest  Mwanossa, ameeleza kuwa baadhi ya  Viongozi waliopewa dhamana ya kujenga na kusimamia miradi ya maendeleo ya  jamii, wameshindwa kuwa wazalendo na kwamba wanatumia madaraka yao vibaya kwa kushindwa kusimamia vema miradi ya maendeleo na rasirimali za taifa.
Kapteni Mwanossa amesema hayo katika maeneo mbalimbali nchini wakati wa mbio za mwenge wa uhuru, baada ya kukagua na kuzindua miradi ya umma na ya mtu binafsi iliyoko Singida na kubaini kuwa miradi ya watu binafsi ina ubora na viwango kuliko miradi ya serikali.

Mwanossa anasema kuwa watu wanaopewa dhamana ya kujenge miradi ya  serikali, hawajengi  katika viwango kama wanavyojenga miradi yao binafsi, na sikuingiza ubinafsi katika miradi ya serikali, kwani  baada kukaguwa majengo mengi ya serikali yalikuwa yako chini ya kiwango na alipowauliza wasimamizi nakukili kuwa yako chini ya kiwango.

No comments: