Tuesday, October 29, 2013

DIWANI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUVUNJA OFISI YA KIJIJI.

Na.Mwadishi wetu
Diwani wa
kata ya Iseke jimbo la Singida magharibi,Bw Emmanuel Jackson amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi mjini Singida  kwa tuhuma za  kuvunja ofisi ya kijiji cha Nkhoiree.

Mbele ya hakimu Asha Mwetindwa mwendesha mashitaka wa serikali,Petrida Muta,alidai tukio lilitokea  septemba 20 mwaka huu saa 8.30 mchana ambapo mshitakiwa alivunja nyumba kwa lengo la kuiba mali

Aidha katika shitaka la pili mtuhumiwa alidaiwa kuwa siku hiyo hiyo mshitakiwa baada ya kuvunja mlango wa nyumba inayotumiwa na serikali ya kijiji cha Nkhoiree,aliiba vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi 298,000.

Vifaa vilivyoibwa ni pamoja , vitabu vya risiti ,hati za malipo, vitabu vya ushuru risiti za zahanati pamoja na  na madumu tupu

Mshitakiwa alikana mashitaka hayo na amerejeshwa rumande hadi kesi hiyo itakapotajwa tena November 11 mwaka huu

No comments: