Tuesday, October 29, 2013

UMUHIMU WA KUCHANGIA UJENZI WA VYUMBA VYA MAABARA SHULENI

Na.Neema Mwampamba
Mkuu wa mkoa wa singida Dr Perseko Korne amewataka wazazi kutoa ushirikiano kwa serikali ili kufanikisha ujenzi wa maabara katika shule za sekondari
Akizugumza na standard radio ofisini kwake Dr Korne amesema ni lazima kila mzazi kuwajibika kwa kutoa mchango wa ujenzi wa maabara ili kuwawezesha wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi kujengewa msingi mzuri
Aidha amesema juhudi zinafanyika ili kuhakikisha maabara za masomo ya Biology Chemia na phizikia zinakamilika katika shule zote ifikapo February 2014
Hata hivyo amewapongeza wakazi wa mkoa wa Singida kwa ushirikiano wanaotoa kwa serikali ili kuhakikisha mpango wa matokeo makubwa sasa unafikiwa.

No comments: